Walawi 8:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
23 Musa akamuchinja. Akatwaa damu ya kondoo huyo na kumupakaa Haruni kwenye incha ya sikio lake la kuume, kidole gumba cha mukono wake wa kuume na cha muguu wake wa kuume.
Nawe utamuchinja na kutwaa sehemu ya damu na kumupakaa Haruni na wana wake kwenye incha za masikio yao ya kuume na vidole gumba vya mikono yao ya kuume, na vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Damu inayobaki utairushia juu ya mazabahu pande zake zote.
Kisha utatwaa sehemu ya damu inayokuwa juu ya mazabahu pamoja na yale mafuta ya kupakaa umunyunyizie Haruni na nguo yake, uwanyunyizie vilevile wana wake na nguo zao. Haruni na wana wake watakuwa wametakaswa kwa ajili yangu pamoja na nguo zao zote.
Kuhani atatwaa sehemu ya damu ya sadaka kwa ajili ya kosa na kumupakaa mutu anayetakaswa katika incha ya sikio lake la kuume na kidole gumba cha mukono wake wa kuume na kidole gumba cha muguu wake wa kuume.
Sehemu ya mafuta yanayobaki katika kigaja chake ataipakaa mutu yule anayetakaswa katika incha ya sikio lake la kuume na kidole gumba cha mukono wake wa kuume na kidole gumba cha muguu wake wa kuume, pahali palepale alipomupakaa damu ya sadaka kwa ajili ya kosa.
Atachinja yule mwana-kondoo dume wa sadaka kwa ajili ya kosa. Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kumupakaa yule mutu anayetakaswa katika incha ya sikio lake la kuume, katika kidole gumba cha mukono wake wa kuume na kidole gumba cha muguu wake wa kuume.
Kuhani atamupakaa yule mutu anayetakaswa mafuta katika incha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mukono wake wa kuume, na kidole gumba cha muguu wake wa kuume. Atamupakaa pahali pale ambapo alimupakaa ile damu ya sadaka kwa ajili ya kosa.
Basi, hii ndiyo sheria kuelekea sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya vyakula, sadaka kwa ajili ya zambi, sadaka kwa ajili ya kosa, kuelekea kutakaswa na kuelekea sadaka ya amani.
Basi wandugu zangu, kufuatana na vile Mungu alivyoonyesha huruma yake kwetu, ninawasihi mujitoe wenyewe kwake kuwa sadaka yenye uzima, takatifu na yenye kumupendeza. Hii ndiyo njia ya kweli ya kumwabudu.
Musitoe tena viungo vya mwili wenu kufanya zambi, mukivitumikisha kama vyombo vya kufanya mabaya. Lakini mujitoe wenyewe kwa kumutumikia Mungu kama watu waliofufuliwa na mutumikishe viungo vya mwili wenu kama vyombo vya kufanya haki.
(Ninatumia luga ya kawaida ya wanadamu kwa sababu ya uzaifu wenu wa kimutu). Zamani mulijitoa kabisa kuwa watumwa wa kufanya mambo machafu na maovu kwa kuishi katika machafuko. Hivi vilevile mujitoe kabisa kuwa watumwa wa kufanya haki kusudi muweze kuishi katika utakatifu.
Tunawaandikia ninyi kanisa la Mungu linalokuwa Korinto, ninyi ambao mumetakaswa kwa njia ya kuungana kwenu na Yesu Kristo na mumeitwa na Mungu kuwa watu wake. Vilevile barua hii ni kwa wote wanaoabudu jina la Bwana Yesu Kristo fasi zote, anayekuwa Bwana wao na Bwana wetu vilevile.
Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.
Kwa maana kama vile ninavyongojea na kutumainia sana, sitafezeheka hata kidogo. Lakini tangia sasa na hata siku zote, nitamutukuza Kristo kwa uhodari katika maisha yangu, ikiwa nitaishi au nitakufa.
Kwa hiyo ilifaa kwamba Mungu aliyeumba vitu vyote na kuvilinda imara, amufanye Yesu kuwa mukamilifu kwa njia ya mateso, kusudi awalete watoto wengi kuwa washiriki wa utukufu wa Mungu. Kwa maana Yesu ndiye anayewaongoza watu wapate kuokoka.