19 Musa akamuchinja na damu ya kondoo huyo akainyunyizia mazabahu pande zake zote.
Makuhani walichinja ngombe dume kwanza, kisha kondoo dume, halafu wana-kondoo na kila mara walitwaa damu ya nyama wale na kuinyunyiza juu ya mazabahu.
Atamuchinjia upande wa kaskazini wa mazabahu, mbele ya Yawe, hao makuhani wazao wa Haruni watainyunyizia mazabahu damu pande zake zote.
Kisha, Musa akaleta kondoo dume wa sadaka ya kuteketezwa. Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo huyo.
Akakata huyo kondoo vipandevipande, akaviteketeza pamoja na kichwa chake na mafuta yake.
Musa akanyunyiza vilevile damu juu ya Hema na juu ya vyombo vyote vya ibada.