Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 8:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kisha Musa akaleta ngombe wa sadaka kwa ajili ya zambi, naye Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha ngombe huyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 8:14
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakutolea sadaka za kuteketezwa za nyama wenye kunona, sadaka za kuteketezwa za kondoo dume; nitatoa sadaka za ngombe dume na beberu.


Yawe alipenda kumuponda kwa mateso. Alitoa uzima wake kwa ajili ya kuondoa zambi. Mutumishi wa Mungu atakuwa na wazao; ataishi maisha marefu. Yeye ndiye atakayetimiza mupango wa Yawe.


Wale makuhani wanaokuwa wa kabila la Lawi ambao ni wazao wa Zadoki, ndio tu watakaokaribia mbele yangu kwa kunitumikia. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Utawapa ngombe dume muchanga kuwa sadaka ya kusamehewa zambi.


Utatwaa damu yake na kuitia juu ya pembe ine za mazabahu na juu ya chongo ine za daraja na juu ya muzunguko wake pande zote. Hivyo ndivyo utakavyoisafisha mazabahu na kuitakasa.


Siku atakapoingia katika patakatifu, katika kiwanja cha ndani kwa kutumika, atatoa sadaka yake ya kusamehewa zambi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


ataweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama wa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, ambayo itakubaliwa kwa ajili ya kumufanyia huyo mutu upatanisho.


Haruni ataweka mikono yake juu ya kichwa cha huyo beberu muzima na kuungama juu yake zambi zote za watu wa Israeli, makosa yao yote na zambi zao zote; naye ataziweka zote juu ya kichwa cha yule mbuzi. Kisha atamwacha huyo beberu aende katika jangwa akipelekwa kule na mutu yeyote anayekuwa tayari.


Haruni atatoa huyo ngombe dume kwa sadaka ya kuondoa zambi kwa ajili yake mwenyewe na kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na jamaa yake.


Wazee wao wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ngombe dume, kisha atachinjwa mbele ya Yawe.


Utwae Haruni na wana wake na zile nguo takatifu, mafuta ya kupakaa, ngombe wa sadaka kwa ajili ya zambi, kondoo dume wawili, na kitunga cha mikate isiyotiwa chachu.


Kisha Walawi wataweka mikono yao juu ya vichwa vya ngombe dume hao; mumoja wao utamutoa kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, na huyo mwingine utamutoa kuwa sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwangu, kwa kuwafanyia Walawi upatanisho.


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ