Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 7:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Hiyo ndiyo sehemu iliyotengwa kwa ajili ya Haruni na wana wake kutoka katika sadaka Yawe anazotolewa kwa moto, tangu siku walipowekwa kuwa makuhani wa Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 7:35
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nawe Musa umulete kwangu Haruni ndugu yako, pamoja na wana wake: Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari. Utawachagua kati ya Waisraeli, kusudi wanitumikie kama vile makuhani.


Haya ndiyo mambo utakayowafanyia Haruni na wana wake kwa kuwatakasa wapate kunitumikia kama vile makuhani. Utatwaa mwana-ngombe dume na kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema,


Kisha utatwaa sehemu ya damu inayokuwa juu ya mazabahu pamoja na yale mafuta ya kupakaa umunyunyizie Haruni na nguo yake, uwanyunyizie vilevile wana wake na nguo zao. Haruni na wana wake watakuwa wametakaswa kwa ajili yangu pamoja na nguo zao zote.


Kisha kufanya hivyo, utatwaa yale mafuta ya kupakaa, umumiminie Haruni juu ya kichwa chake kwa kumutakasa.


Wakati huo, muzigo waliowabebesha atauondoa na nira waliyowatia kwenye shingo lenu itavunjwa. Adui amepanda kutoka Rimoni,


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Halafu Musa akatwaa mafuta ya kupakaa na damu kutoka mazabahu akamunyunyizia Haruni na wana wake hata na nguo zao vilevile. Hivyo Musa akamutakasa Haruni na wana wake pamoja na nguo zao.


Aliyetumwa na Mungu anasema maneno ya Mungu, kwa sababu Mungu anamujaza Roho wake kwa uwingi.


Ni Mungu mwenyewe ndiye anayetuimarisha pamoja nanyi katika ushirika na Kristo, na ni yeye mwenyewe ndiye aliyetuchagua.


Lakini munajazwa na Roho Mutakatifu ambaye Kristo alimimia juu yenu, na kwa hiyo ninyi wote munajua ukweli.


Lakini Kristo amemimia Roho juu yenu. Na kufuatana na vile Roho yule anavyokaa ndani yenu, hamuhitaji kufundishwa na mutu, kwa maana Roho wake anawafundisha mambo yote. Roho yule anasema ukweli wala hasemi uongo. Basi kama vile Roho alivyowafundisha, mukae ndani ya Kristo.


Kati ya makabila yote ya Israeli nilimuchagua Haruni na jamaa yake kuwa makuhani wangu, wanitumikie kwenye mazabahu, wafukize ubani na kuvaa kizibao mbele yangu. Nikaipatia jamaa ya babu yako sadaka zangu ambazo Waisraeli walinitolea kwa moto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ