Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 7:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Muguu wa kuume wa nyuma wa nyama wa sadaka zenu za amani mutamupa kuhani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 7:32
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kuhani anapotakaswa, kilali na paja la kondoo dume wa utakaso vitaletwa na kutakaswa mbele yangu kwa kufanya kitambulisho cha kunitolea, navyo vitakuwa vya Haruni na wana wake.


Lakini kilali ambacho wanafanya nacho kitambulisho cha kumutolea Yawe na muguu unaotolewa sadaka kama vile kitambulisho, munaweza kuvikulia pahali popote pasipo kuwa pachafu. Utakula wewe na watoto wako wanaume na wanawake. Vitu hivyo umepewa kama haki yako na ya wazao wako kutoka sadaka za amani za watu wa Israeli.


Muguu huo utakuwa mali ya kuhani anayekuwa muzao wa Haruni anayetolea damu ya sadaka za amani na mafuta yake.


Yawe amewaagiza watu wa Israeli watenge kilali hicho na muguu huo wa nyama wa sadaka zao za amani, wamupe kuhani Haruni na wazao wake, maana sehemu hiyo imewekewa kwa hao makuhani milele.


Lakini vile vilali na ule muguu wa nyuma wa kuume, Haruni akafanya navyo kitambulisho cha kumutolea Yawe, kama vile Musa alivyoamuru.


Kila sadaka ya matoleo yote matakatifu ya Waisraeli watakayomuletea kuhani, itakuwa yake.


Halafu kuhani atavitikisa vitu hivyo kama sadaka ya kutikisa mbele ya Yawe; vyote hivi ni sehemu takatifu kwa kuhani, pamoja na kilali kilichotikiswa na paja lililotolewa kama sadaka. Nyuma ya hayo yote, munaziri anaweza kunywa divai.


“Na hii itakuwa haki ya makuhani kutoka kwa watu wanaotolea sadaka ikuwe ni ngombe au kondoo: watamupa kuhani muguu wa mbele, mashavu na matumbotumbo.


Yule mupishi akaenda akaleta paja na sehemu ya nyama iliyokuwa upande wa juu wa paja hilo na kuviweka mbele ya Saulo. Halafu Samweli akamwambia Saulo: “Angalia kile ulichowekewa; sasa kimewekwa mbele yako. Sasa ukule kwa sababu kimewekwa kwa ajili yako kusudi upate kula pamoja na wageni.” Hivyo, Saulo akakula pamoja na Samweli siku hiyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ