Wazao wa Haruni wataiteketeza juu ya mazabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa inayokuwa juu ya kuni. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.
Basi, kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi, naye atasamehewa. Unga unaobaki utakuwa wa kuhani kama vile inavyofanyika juu ya sadaka ya ngano.
Yawe amewaagiza watu wa Israeli watenge kilali hicho na muguu huo wa nyama wa sadaka zao za amani, wamupe kuhani Haruni na wazao wake, maana sehemu hiyo imewekewa kwa hao makuhani milele.
Kisha Musa akatwaa kile kilali na kufanya kitambulisho cha kumutolea Yawe. Sehemu hiyo ya yule kondoo dume wa utakaso ni mali ya Musa kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
Vilevile, vitu vingine vyote Waisraeli watakavyonitolea kama vile sadaka za kutikiswa, vitakuwa vyako. Ninakupa wewe, wana wako na wabinti zako kuwa haki yenu milele. Mutu yeyote katika jamaa yako asiyekuwa muchafu anaweza kula vitu hivyo.
Munajua hakika kuwa wale wanaotumika katika hekalu wanapata chakula chao ndani ya hekalu. Na wale wanaotumika kwa kutoa sadaka juu ya mazabahu wanapata sehemu yao kutoka sadaka zile.