Kama mutu yeyote wa jamii ya Israeli au mugeni anayeishi kati yao anakula damu yoyote, mimi nitamukasirikia mutu yule aliyekula damu na kumutenga mbali na watu wake.
Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?
Watu wengine wakamwambia Saulo: “Angalia watu wanatenda zambi mbele ya Yawe kwa kula nyama yenye damu.” Saulo akawaambia watu: “Ninyi ni waasi. Muviringishe jiwe kubwa na kulileta hapa.”