Basi, kuhani atanyunyizia damu kwenye mazabahu ya Yawe inayokuwa kwenye mulango wa hema la mukutano na kuteketeza yale mafuta yakuwe harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.
Maana mioyo ya watu hawa imegeuka kuwa migumu, wameziba masikio yao na wamefunga macho yao. Isingekuwa hivi, wangeona na macho yao, wangesikia na masikio yao, wangefahamu na mioyo yao, na wangegeukia kwangu na ningewaponyesha.
Kwa nini basi, umezionea wivu matoleo na sadaka nilizowaamuru watu waniletee, nawe ukawaheshimu watoto wako kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu nzuri za sadaka ambazo watu wangu wa Israeli wananitolea?