Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 7:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Mutu yeyote anayegusa kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, au kitu cha mutu kinachohesabiwa kuwa kichafu, au nyama anayehesabiwa kuwa muchafu, au kitu chochote kinahesabiwa kuwa kichafu ambacho ni chukizo, akikula nyama ya sadaka ya amani Yawe aliyotolewa, mutu huyo atatengwa na watu wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 7:21
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mwanaume yeyote asiyetahiriwa atatengwa na watu, maana atakuwa amevunja agano langu.”


Yawe akaendelea kusema: “Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutaondoa chachu katika nyumba zenu. Mutu yeyote akikula kitu kilichotiwa chachu katika muda ule wa siku saba, anapaswa kuondolewa kati ya Waisraeli.


Katika siku hizo saba, musikuwe na chachu yoyote katika nyumba zenu. Mutu yeyote, akuwe mugeni au mwenyeji, akikula kitu kilichotiwa chachu, ataondolewa katika kusanyiko la Waisraeli.


Basi, uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninyi munakula nyama yenye damu, munaziabudu sanamu za miungu yenu na kumwanga damu! Munazani kwamba mutapewa inchi hii ikuwe yenu?


Halafu nikamwambia hivi: Ee, Bwana wangu Yawe, sijajichafua hata kidogo kwa kula nyamafu wala nyama aliyeuawa na nyama wa pori, wala sijapata kuonja nyama anayehesabiwa kuwa muchafu tangu ujana wangu.


Wadudu wote wenye mabawa na wanaotembea kwa miguu mine, hao ni wachafu kwenu.


Kama mutu yeyote wa jamii ya Israeli au mugeni anayeishi kati yao anakula damu yoyote, mimi nitamukasirikia mutu yule aliyekula damu na kumutenga mbali na watu wake.


Maana, uzima wa kila kiumbe uko katika damu. Ndiyo maana nimewaagiza Waisraeli, wasikule damu ya kiumbe chochote maana uzima wa kiumbe chochote ni damu yake. Yeyote atakayekula damu atatengwa.


Watu wote watakaofanya mambo hayo ya kuchukiza wanapaswa kutengwa mbali na watu wao.


Naye atakayekula nyama hiyo anapaswa kubeba lazima ya uovu wake kwa sababu amechafua kitu kitakatifu cha Yawe. Mutu huyo atatengwa na watu wake.


Mimi mwenyewe nitamukasirikia mutu huyu na kumutenga na watu wake kwa sababu alimutoa mumoja wa watoto wake sadaka kwa mungu Moleki na hivyo akachafua Pahali pangu Patakatifu na jina langu takatifu.


Uwaambie hivi: Kama mumoja wa wazao wenu katika vizazi vyenu vyote akikaribia vitu vitakatifu ambavyo Waisraeli wamevitakasa kwa ajili yangu mimi Yawe akiwa muchafu, mutu huyu atatengwa nami. Mimi ni Yawe.


Mutu yeyote wa kizazi cha Haruni akiwa na ugonjwa wa ukoma au anatokwa usaha asikule vitu vitakatifu mpaka atakapokuwa safi. Mutu yeyote akigusa mutu aliyejichafua kwa kugusa maiti au mutu aliyetokwa na mbegu za uzazi,


Mutu yeyote asiyefunga kula siku hiyo ni lazima atengwe mbali na watu wake.


iliyotolewa sadaka ya amani kwa Yawe. Lakini mutu yeyote anayehesabiwa kuwa muchafu akikula nyama hiyo, atatengwa na watu wake.


Mutu yeyote akikula mafuta ya nyama aliyetolewa kwa Yawe kwa moto, atatengwa na watu wake.


Mutu yeyote akikula damu yoyote, atatengwa na watu wake.


Chochote mutu muchafu atakachogusa kitakuwa kichafu, na yeyote atakayekigusa kitu hicho atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Lakini kiumbe chochote kinachoishi ndani ya maji kisichokuwa na mapezi wala magamba musikule; hivyo ni vichafu kwenu.


Siku hiyo, Saulo hakusema neno lolote, maana alifikiri kwamba labda Daudi amepatwa na tatizo au yeye si safi kwa kuhuzuria sikukuu hiyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ