Walawi 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
2 Nyama wa sadaka kwa ajili ya kosa atachinjiwa pahali wanapochinjiwa nyama wa sadaka za kuteketezwa kwa moto na damu yake itanyunyizwa juu ya mazabahu pande zake zote.
Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi. Wafalme watapumbazika kwa sababu yake, maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa, na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.
Halafu katika baraza karibu na njia kulikuwa meza mbili upande mumoja na zingine mbili upande mwingine. Meza hizo zilitumika kuwa pahali pa kuchinjia sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya usamehe wa zambi na sadaka ya malipo ya kosa.
Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;
Kisha, atamuchinja huyo ngombe mbele ya Yawe. Nao makuhani wazao wa Haruni wataichukua damu na kuinyunyizia mazabahu inayokuwa kwenye mulango wa hema la mukutano, pande zake zote.
Kisha atachinja yule mwana-kondoo katika Pahali Patakatifu, wanapochinjia nyama wa sadaka kwa ajili ya zambi na sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Sadaka hii kwa ajili ya kosa na vilevile sadaka kwa ajili ya zambi, ni mali ya kuhani. Ni sadaka takatifu kabisa.
Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja kwenye mulango wa hema la mukutano. Hao makuhani wazao wa Haruni watainyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.
akiweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja mbele ya hema la mukutano. Makuhani wazao wa Haruni watanyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.
Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha beberu na kumuchinjia pahali wanapochinjia sadaka za kuteketezwa mbele ya Yawe. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi.
Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha mwana-kondoo huyo wa sadaka kwa ajili ya zambi na kumuchinjia pahali pale wanapochinjia nyama wa sadaka za kuteketezwa.
Zaidi ya hayo, yule mutu atalipa hasara yote aliyosababisha juu ya vitu vitakatifu kwa kuongeza sehemu moja ya tano ya bei yake na kumupatia kuhani yote. Basi, kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi kwa huyo kondoo dume anayekuwa sadaka kwa ajili ya kosa, naye atasamehewa.
Lakini kama hawezi kutoa mwana-kondoo wa sadaka ya kosa kwa ajili ya zambi aliyotenda, basi atamuletea Yawe hua wawili au vitoto viwili vya njiwa, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto.
na kujitakasa kwa Yawe kwa siku zake za kujitenga. Hizo siku za kwanza hazitahesabiwa kwa sababu nywele zake zilizokuwa zimetakaswa zimechafuka. Atatoa mwana-kondoo dume wa mwaka mumoja kuwa sadaka ya kosa.
Kwa njia ya imani, alianzisha sikukuu ya Pasaka, na kuamuru damu inyunyizwe, kusudi malaika mwangamizaji asiwaue wazaliwa wa kwanza wanaume wa Waisraeli.
Mungu Baba aliwachagua ninyi tangu mbele kufuatana na mupango wake na kufanywa watakatifu na Roho, mupate kumutii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Ninawatakia neema na amani kwa uwingi.