15 Nyama ya sadaka hiyo ya amani ya kumushukuru Mungu itakuliwa siku hiyohiyo inapotolewa. Hataacha hata sehemu yake mpaka asubui.
Vilevile musiache nyama yoyote mpaka asubui. Nyama yoyote itakayobaki mpaka asubui mutaiteketeza kwa moto.
Usinitolee damu ya sadaka yangu pamoja na mukate uliotiwa chachu, wala usiyaache mafuta ya sikukuu yangu yabaki mpaka asubui.
Ikiwa mutu anatoa sadaka hiyo kwa kumushukuru Mungu, basi, ataitoa pamoja na maandazi yasiyotiwa chachu yaliyopakwa mafuta, mikate myembamba iliyopakwa mafuta na maandazi ya unga laini uliochanganywa na mafuta.
Kila mwaka, wewe na jamaa yako mutakula nyama hao mbele ya Yawe, Mungu wenu, pahali Yawe atakapochagua.