Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 7:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Pamoja na sadaka yake hiyo ya amani ya kumushukuru Mungu, ataleta maandazi yaliyotiwa chachu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 7:13
7 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Unaweza kumuletea Yawe mazao yako ya kwanza kama sadaka. Lakini hayo hayatatolewa kwenye mazabahu kama harufu ya kumupendeza.


Kila jamaa italeta mikate miwili ya sadaka ya kutoa kwa kitambulisho mbele yangu mimi Yawe. Kila mukate utatengenezwa kwa kilo mbili za unga laini uliotiwa chachu na huo mutanitolea mimi Yawe ukiwa ni matoleo ya malimbuko yenu.


Pamoja na hayo, mutatoa wana-kondoo saba wa mwaka mumoja, mwana-ngombe dume mumoja, na kondoo dume wawili. Nyama hao watakuwa sadaka ya kuteketezwa pamoja na sadaka ya vyakula na sadaka za kinywaji. Harufu ya sadaka hizi itanipendeza mimi Yawe.


Mutoe sadaka ya shukrani ya mikate isiyotiwa chachu. Mutangaze popote kwamba mumetoa kwa mapenzi; maana ndivyo munavyopenda kufanya! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Yesu akawaambia tena mufano mwingine, akisema: “Ufalme wa mbinguni unafanana na chachu mwanamuke mumoja aliyoitwaa na kuichanga na vipimo vitatu vya unga kwa kuponda mikate hata yote ikapata kuvimba.”


Kila kitu Mungu alichokiumba ni kizuri, wala hakuna kile kinachopaswa kukataliwa, lakini inafaa kumushukuru Mungu mbele ya kukikula.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ