Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 6:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Hii ndio sheria juu ya ibada inayoelekea sadaka ya vyakula. Wazao wa Haruni ndio wanaokuwa na uwezo wa kumutolea Yawe sadaka hiyo juu ya mazabahu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 6:7
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anawatendea mema maelfu, anawasamehe uovu, makosa na zambi. Lakini hataacha kumwazibu mwenye kosa. Anawalipiza watoto na wajukuu uovu wa baba na babu zao, hata kizazi cha tatu na cha ine.


Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.


Na mutu mwovu akiacha uovu wake, akianza kutenda mambo ya haki na mema ataishi kwa sababu ya matendo yake mema.


Mutu yeyote akileta sadaka ya ngano kwa Yawe, sadaka hiyo ikuwe ya unga laini. Atautia mafuta na ubani.


Kwa hiyo atamufanya ngombe dume huyu kama alivyomufanya yule mwingine wa sadaka kwa ajili ya zambi. Basi, huyo kuhani atawafanyia watu ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi, nao watasamehewa.


Mafuta yote ya beberu huyo atayateketeza juu ya mazabahu, kama vile anavyofanya na mafuta ya nyama wa sadaka ya amani. Kwa hiyo kuhani atamufanyia mutawala ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.


Mafuta yote ya mbuzi huyo atayaondoa kama vile anavyoondoa mafuta ya nyama wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya mazabahu, na harufu yake nzuri itamupendeza Yawe. Basi, kuhani atamufanyia yule mutu hiyo ibada ya upatanisho, naye atasamehewa.


Kisha atamutoa yule wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa kulingana na maagizo. Kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.


Basi, kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi, naye atasamehewa. Unga unaobaki utakuwa wa kuhani kama vile inavyofanyika juu ya sadaka ya ngano.


Atamuletea kuhani kondoo dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake ikiwa na bei sawa na ile ya sadaka ya kosa. Na kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa kosa alilofanya, naye atasamehewa.


Mumoja wa makuhani atatwaa mukono mumoja wa unga wa sadaka ya vyakula pamoja na mafuta na ubani wote na kuviteketeza juu ya mazabahu kama vile sehemu ya ukumbusho. Harufu yake itamupendeza Yawe.


Nyama wa sadaka kwa ajili ya kosa atachinjiwa pahali wanapochinjiwa nyama wa sadaka za kuteketezwa kwa moto na damu yake itanyunyizwa juu ya mazabahu pande zake zote.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Kwa hiyo ninawaambia: watu wataweza kusamehewa zambi zote wanazofanya na matusi yao yote. Lakini mutu anayetukana Roho Mutakatifu hatasamehewa.


Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.


Lakini tukiitikia zambi zetu mbele ya Mungu, yeye atatusamehe zambi zetu na kutusafisha toka katika maovu yote kwa maana yeye ni mwaminifu na mwenye haki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ