Yawe alipenda kumuponda kwa mateso. Alitoa uzima wake kwa ajili ya kuondoa zambi. Mutumishi wa Mungu atakuwa na wazao; ataishi maisha marefu. Yeye ndiye atakayetimiza mupango wa Yawe.
Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha beberu na kumuchinjia pahali wanapochinjia sadaka za kuteketezwa mbele ya Yawe. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi.
Ikiwa kuhani ambaye amepakwa mafuta ndiye aliyetenda zambi hata akawatia watu katika kosa, basi huyo atamutolea Yawe ngombe dume muchanga asiyekuwa na kilema akuwe sadaka kwa ajili ya zambi.
Usipikwe hata kidogo pamoja na chachu. Nimewapa wao sehemu hiyo kutoka sadaka wanazonitolea kwa moto. Ni sadaka takatifu kabisa kama vile sadaka kwa ajili ya zambi na kwa ajili ya kosa zinavyokuwa.
Wazao wanaume wa Haruni ndio peke yao wanaoruhusiwa kula sehemu hiyo maana hiyo imetengwa siku zote kwa ajili yao kutoka sadaka Yawe anazotolewa kwa moto. Yeyote atakayezigusa atakuwa mutakatifu.
Lakini kama damu ya sadaka yoyote kwa ajili ya zambi imeletwa ndani ya hema la mukutano kwa kufanya ibada ya upatanisho katika Pahali Patakatifu, sadaka hiyo itateketezwa kwa moto.
Kisha kusafisha matumbotumbo na miguu kwa maji, Musa akaviteketeza vyote juu ya mazabahu pamoja na sehemu zingine za huyo kondoo kama sadaka ya kuteketezwa. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto, yenye harufu ya kumupendeza Yawe. Musa akafanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
(Watu wa Israeli wakasafiri kutoka visima vya watu wa Yakani mpaka Musara. Haruni akakufa na kuzikwa kule. Eleazari mwana wake, akatwaa nafasi yake kama vile kuhani.