Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 6:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Kuhani anayekuwa muzao wa Haruni ambaye amepakwa mafuta kushika nafasi yake atamutolea Yawe sadaka hiyo. Hilo ni agizo la milele. Sadaka yote itateketezwa kwa moto.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 6:15
5 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hiyo itakuwa ndani ya hema la mukutano inje ya pazia lile mbele ya Sanduku la Agano na Haruni na wana wake wataitunza mbele yangu tangu magaribi mpaka asubui. Sharti hili lifuatwe siku zote na Waisraeli wote, kizazi kwa kizazi.


Kisha, atawaletea hao makuhani, wazao wa Haruni. Atatwaa mukono mumoja wa unga huo laini wenye mafuta na ubani na kumupelekea kuhani mumoja ambaye atauteketeza juu ya mazabahu ukuwe sadaka ya ukumbusho kwa Yawe. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Kuhani atatwaa sehemu ya sadaka hiyo ikiwa ni sadaka ya ukumbusho na kuiteketeza juu ya mazabahu. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Ndiyo maana munapaswa kufuata sharti hili siku zote na pahali popote mutakapokaa. Musikule hata kidogo mafuta wala damu.


Unga huo utachanganywa na mafuta na kupikwa juu ya kikaango. Kisha utauleta ukiwa vipandevipande na kumutolea Yawe na harufu ya sadaka yake itamupendeza Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ