Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 6:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Tangu wakati wa kutakaswa kwa Haruni na wazao wake wanapaswa kumutolea Yawe kilo moja ya unga laini kwa siku, nusu moja ya unga huo ataitoa asubui na nusu ingine magaribi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 6:13
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Haya ndiyo mambo utakayowafanyia Haruni na wana wake kwa kuwatakasa wapate kunitumikia kama vile makuhani. Utatwaa mwana-ngombe dume na kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema,


mikate isiyotiwa chachu, maandazi yasiyotiwa chachu yaliyopondwa kwa mafuta, na mikate myembamba isiyotiwa chachu, lakini iliyopakwa mafuta. Vyote hivi vikuwe vimetengenezwa kwa unga laini wa ngano.


Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza, utatoa kilo moja ya unga laini uliochanganywa na litre moja ya mafuta safi, na litre moja ya divai kama sadaka ya kinywaji.


Mufalme wao atatoroka kwa ajili ya hofu, na wakubwa wao wataiacha bendera yao kwa ajili ya woga. –Ni ujumbe wa Yawe ambaye moto wake uko katika Sayuni, ambaye furu lake liko katika Yerusalema.


na chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wanaotumika kwenye mazabahu. Makuhani hawa ni wale wa ukoo wa Zadoki, ndio hao kati ya watu wa kabila la Lawi wanaoruhusiwa kwenda mbele ya Yawe.


Unga huo utachanganywa na mafuta na kupikwa juu ya kikaango. Kisha utauleta ukiwa vipandevipande na kumutolea Yawe na harufu ya sadaka yake itamupendeza Mungu.


Unga uliobakia Haruni na wazao wake makuhani wataukula bila kutiwa chachu. Wataukula kwenye Pahali Patakatifu katika kiwanja cha hema la mukutano.


Yawe akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya mazabahu. Watu wote walipoona huo moto wakapiga vigelegele na kuinama uso mpaka chini.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ