Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 5:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Au kama mutu yeyote kati yenu akijichafua bila kukusudia kwa kugusa kitu chochote kichafu, ikuwe ni muzoga wa nyama wa pori au wa kufugwa au wadudu, atakuwa na kosa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 5:2
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yananifundisha mimi mutumishi wako; kuyafuata kunaniletea zawadi kubwa.


Muondoke! Muondoke! Mutoke pale! Musiguse kitu chochote kichafu! Muondoke kule Babeli! Mujitakase, enyi munaobeba vyombo vya Yawe.


Viumbe hivyo vitakuwa siku zote vichafu kwenu. Musikule nyama yao, wala musiguse mizoga yao maana ni chafu.


Kwa sababu nyama hao ni wachafu, musikule nyama yao wala musiguse mizoga yao.


Ikiwa Waisraeli wote pamoja wametenda zambi bila kukusudia kwa kufanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe,


Mutu yeyote akitenda zambi bila kujua, kwa kuvunja amri yoyote ya Yawe, yeye ana kosa, na atalipa azabu ya kosa lake.


Au mutu akigusa kitu chochote toka kwa mwanadamu kinachohesabiwa kuwa kichafu, kikuwe kile ambacho kinamufanya mutu kuwa muchafu bila kujua, basi, atakapojua atakuwa na kosa.


Au, kama mutu akiapa kufanya kitu chochote, chema au kibaya, kama vile watu wanavyofanya bila kufikiri, atakapojua atakuwa na kosa.


Mutu yeyote anayegusa kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, au kitu cha mutu kinachohesabiwa kuwa kichafu, au nyama anayehesabiwa kuwa muchafu, au kitu chochote kinahesabiwa kuwa kichafu ambacho ni chukizo, akikula nyama ya sadaka ya amani Yawe aliyotolewa, mutu huyo atatengwa na watu wake.


Hagai akawauliza tena: Mutu anayehesabiwa kuwa muchafu kwa kugusa maiti, akigusa sehemu ya vyakula hivi, chakula hicho kitakuwa kichafu? Makuhani wakamujibu: Ndiyo, kitakuwa kichafu.


Chochote mutu muchafu atakachogusa kitakuwa kichafu, na yeyote atakayekigusa kitu hicho atakuwa muchafu mpaka magaribi.


Ole kwenu! Munafanana na makaburi yasiyoonekana wazi ambayo watu wanatembea juu yao pasipo kujua.”


Kwa sababu hiyo Bwana anasema: “Mutoke kati yao, mujitenge nao. Musiguse kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, nami nitawapokea.


Vilevile musikule nguruwe, maana ijapokuwa kwato zake zinagawanyika sehemu mbili, yeye hacheui; hao ni wachafu kwenu. Musikule nyama zao wala musiguse mizoga yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ