Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 5:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Zaidi ya hayo, yule mutu atalipa hasara yote aliyosababisha juu ya vitu vitakatifu kwa kuongeza sehemu moja ya tano ya bei yake na kumupatia kuhani yote. Basi, kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi kwa huyo kondoo dume anayekuwa sadaka kwa ajili ya kosa, naye atasamehewa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 5:16
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninaregea kwa ajili ya kulalamika, na koo langu limekauka. Macho yangu yamefifia, nikikungojea ewe Mungu wangu.


Mwizi akikamatwa yuko anavunja nyumba, naye akipigwa na kufa, aliyemwua hana kosa la mauaji.


Kama mutu mwingine akikula chakula kitakatifu bila kujua, basi, atalipa nyongezo ya sehemu moja ya tano pamoja na kipimo sawasawa alichokula na kumurudishia kuhani.


Lakini ikiwa mwenyeji anataka kumukomboa, basi, ataongeza asili mia makumi mbili ya bei ya nyama huyo.


Kama huyo mutu aliyeitakasa akitaka kuikomboa hiyo nyumba, basi, ataongeza asili mia makumi mbili ya bei yake, nayo itakuwa mali yake.


Kama ni nyama muchafu, mwenyeji atamununua kwa kulingana na jinsi munavyomupima na ataongeza asili mia makumi mbili ya bei ya nyama huyo. Kama hakombolewi, basi atauzishwa kulingana na vipimo vyenu.


Kama mutu akitaka kukomboa zaka yake, atalipa bei yake na kuongeza asili mia makumi mbili ya bei ya zaka hiyo.


Kwa hiyo atamufanya ngombe dume huyu kama alivyomufanya yule mwingine wa sadaka kwa ajili ya zambi. Basi, huyo kuhani atawafanyia watu ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi, nao watasamehewa.


Mafuta yote ya beberu huyo atayateketeza juu ya mazabahu, kama vile anavyofanya na mafuta ya nyama wa sadaka ya amani. Kwa hiyo kuhani atamufanyia mutawala ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.


Kisha atamutoa yule wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa kulingana na maagizo. Kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.


Basi, kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi, naye atasamehewa. Unga unaobaki utakuwa wa kuhani kama vile inavyofanyika juu ya sadaka ya ngano.


na kumuletea Yawe sadaka yake kwa ajili ya kosa. Kwa ajili ya zambi aliyotenda ataleta kondoo dike au mbuzi dike kutoka kundi lake amutoe sadaka kwa ajili ya zambi. Naye kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake.


Nyama wa sadaka kwa ajili ya kosa atachinjiwa pahali wanapochinjiwa nyama wa sadaka za kuteketezwa kwa moto na damu yake itanyunyizwa juu ya mazabahu pande zake zote.


Anapaswa kutubu zambi yake aliyotenda; na atatoa malipo kamilifu kwa kosa lake, akiongeza asilimia makumi mbili ya malipo hayo; atatoa malipo hayo kwa yule aliyemukosea.


Lakini ikiwa mutu huyo amekufa na hana ndugu wa karibu ambaye anaweza kupokea malipo hayo, basi, malipo ya kosa yatatolewa kwa Yawe kwa ajili ya makuhani; malipo haya ni pamoja na kondoo dume wa upatanisho ambaye atatumiwa kwa kumufanyia upatanisho kwa ajili ya zambi yake.


Lakini Zakayo akasimama mbele ya Bwana na kumwambia: “Bwana! Ninawapa masikini nusu ya mali zangu, na kama nimetwaa kitu cha mutu kwa kumudanganya, nitamurudishia mara ine sawa na kitu kile.”


Lakini kwanza nilihubiri wakaaji wa Damasiki, na wa Yerusalema na wa jimbo lote la Yudea nao watu wa mataifa mengine vilevile. Nilihubiri kwao kwamba wageuke toka zambi zao na kumurudilia Mungu, nao waonyeshe kwa njia ya matendo yao kwamba wamegeuka.


Wao wakawaambia: “Mukirudisha Sanduku la Mungu wa Israeli, musilirudishe mikono mitupu. Lakini munapolirudisha mupeleke na sadaka ya malipo ya kosa kwa kuondoa makosa yenu. Mukifanya hivyo mutapona, nanyi mutafahamu kwa nini amekuwa akiwaazibu kwa mufululizo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ