Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 4:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kufukizia ubani wenye harufu nzuri, mbele ya Yawe katika hema la mukutano. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 4:7
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe ni Mungu; yeye ametujalia mwangaza wake. Mushike matawi katika mikono, mukiandamana mpaka kwenye mazabahu.


Utatwaa sehemu ya damu na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu kwa kidole chako, na damu yote inayobaki utaimwanga chini ya mazabahu.


Kisha, atamuchinja huyo ngombe mbele ya Yawe. Nao makuhani wazao wa Haruni wataichukua damu na kuinyunyizia mazabahu inayokuwa kwenye mulango wa hema la mukutano, pande zake zote.


Kisha atatoka na kwenda kwenye mazabahu inayokuwa mbele ya Yawe na kufanya ibada ya upatanisho. Atatwaa sehemu ya damu ya yule ngombe dume na ya yule mbuzi na kupakaa pembe za mazabahu pande zote.


Kisha, sehemu ya damu atazipakaa kwenye pembe za mazabahu inayokuwa katika hema la mukutano mbele ya Yawe. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.


Kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka kwa ajili ya zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka.


Kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka ya kuondoa zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu iliyobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu.


Kisha kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka kwa ajili ya zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu.


Sehemu ya damu yake ataipakaa pembeni ya mazabahu na ile ingine ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi.


Musa akamuchinja huyo ngombe, akatwaa damu akapakaa pembe za mazabahu pande zote kwa kidole chake kwa kuitakasa. Kisha akatwaa damu iliyobaki akaimwanga chini kwenye tako la mazabahu ambayo alitakasa kwa kuifanyia ibada ya upatanisho.


Wana wake wakamuletea damu, naye akachovya kidole chake katika damu hiyo na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu. Damu iliyobakia akaimwanga kwenye tako la mazabahu.


Lakini sasa, katika kuungana kwenu na Yesu Kristo, ninyi muliokuwa mbali, mumekuwa karibu kwa njia ya damu ya Kristo.


Kwa sababu hii, Kristo ni mupatanishi wa agano jipya. Kwa njia ya kufa kwake aliwakomboa watu toka katika makosa waliyofanya chini ya uongozi wa agano la kwanza, kusudi wale walioalikwa na Mungu wapate kupokea urizi wa milele aliowaahidia.


Musa akanyunyiza vilevile damu juu ya Hema na juu ya vyombo vyote vya ibada.


Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tano, nikaona chini ya mazabahu, roho za watu waliouawa kwa sababu ya kutangaza Neno la Mungu na kwa sababu ya ushuhuda wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ