Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 4:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Kisha kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka kwa ajili ya zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 4:34
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa ajili ya uaminifu wake, Yawe, alipenda kutukuza sheria yake na kuiheshimisha.


Kisha, sehemu ya damu atazipakaa kwenye pembe za mazabahu inayokuwa katika hema la mukutano mbele ya Yawe. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.


Kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka kwa ajili ya zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka.


Kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka ya kuondoa zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu iliyobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu.


Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kufukizia ubani wenye harufu nzuri, mbele ya Yawe katika hema la mukutano. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.


Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa.


Kwa maana kwa njia ya Kristo, Sheria imepata kufikia ukomo wake kusudi kila mutu anayeamini apate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.


Basi sasa hakuna azabu kwa wale wanaoungana na Yesu Kristo.


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Kwa hiyo ilifaa kwamba Mungu aliyeumba vitu vyote na kuvilinda imara, amufanye Yesu kuwa mukamilifu kwa njia ya mateso, kusudi awalete watoto wengi kuwa washiriki wa utukufu wa Mungu. Kwa maana Yesu ndiye anayewaongoza watu wapate kuokoka.


Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ