Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 4:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Mafuta yote ya beberu huyo atayateketeza juu ya mazabahu, kama vile anavyofanya na mafuta ya nyama wa sadaka ya amani. Kwa hiyo kuhani atamufanyia mutawala ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 4:26
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, wale makuhani wakawachinja, na kunyunyiza damu yao juu ya mazabahu kusudi ikuwe sadaka ya upatanisho kwa Waisraeli wote, kwa maana mufalme Hezekia alikuwa ameagiza sadaka ya kuteketeza kwa moto na sadaka ya maondoleo itolewe kwa ajili ya Waisraeli wote.


Kesho yake, utatoa beberu asiyekuwa na kilema, kuwa sadaka ya kusamehewa zambi; mazabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa damu ya ngombe dume.


ataweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama wa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, ambayo itakubaliwa kwa ajili ya kumufanyia huyo mutu upatanisho.


Kama hawezi kutoa mwana-kondoo, basi, ataleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa; mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya zambi. Kuhani atamufanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.


Yale mafuta yaliyobaki atayapakaa yule mutu kwenye kichwa. Hivyo kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho mbele ya Yawe.


Kuhani atatoa hao, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kuhani atamufanyia mutu huyu ibada ya upatanisho mbele ya Yawe na kumwondolea uchafu wake wa kutokwa na usaha.


Itakuwa hivyo kwa sababu uzima wa kiumbe uko katika damu. Nimewaagiza kutolea damu kwenye mazabahu kwa kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya roho zenu, kwa sababu damu inafanya upatanisho, nao uzima uko katika damu.


Kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa kutumia kondoo huyo mbele ya Yawe kwa ajili ya zambi aliyotenda, naye atasamehewa zambi hiyo aliyotenda.


Wazao wa Haruni wataiteketeza juu ya mazabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa inayokuwa juu ya kuni. Hiyo ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri ya kumupendeza Yawe.


Mafuta yote ya nyama huyo atayatwaa na kuyateketeza kwenye mazabahu.


Kwa hiyo atamufanya ngombe dume huyu kama alivyomufanya yule mwingine wa sadaka kwa ajili ya zambi. Basi, huyo kuhani atawafanyia watu ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi, nao watasamehewa.


Mafuta yote ya mbuzi huyo atayaondoa kama vile anavyoondoa mafuta ya nyama wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya mazabahu, na harufu yake nzuri itamupendeza Yawe. Basi, kuhani atamufanyia yule mutu hiyo ibada ya upatanisho, naye atasamehewa.


Kisha ataondoa mafuta yote kama vile anavyoondoa mafuta ya mwana-kondoo wa sadaka ya amani na kuhani atayateketeza juu ya mazabahu, pamoja na sadaka zinazotolewa kwa Yawe kwa moto. Kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.


Kisha atamutoa yule wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa kulingana na maagizo. Kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.


Basi, kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi, naye atasamehewa. Unga unaobaki utakuwa wa kuhani kama vile inavyofanyika juu ya sadaka ya ngano.


Zaidi ya hayo, yule mutu atalipa hasara yote aliyosababisha juu ya vitu vitakatifu kwa kuongeza sehemu moja ya tano ya bei yake na kumupatia kuhani yote. Basi, kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi kwa huyo kondoo dume anayekuwa sadaka kwa ajili ya kosa, naye atasamehewa.


Atamuletea kuhani kondoo dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake ikiwa na bei sawa na ile ya sadaka ya kosa. Na kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa kosa alilofanya, naye atasamehewa.


Hii ndio sheria juu ya ibada inayoelekea sadaka ya vyakula. Wazao wa Haruni ndio wanaokuwa na uwezo wa kumutolea Yawe sadaka hiyo juu ya mazabahu.


Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya Waisraeli wote pamoja, nao watasamehewa kwa sababu si kosa lililokusudiwa, na wameleta sadaka yao, sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe kama sadaka ya zambi kwa ajili ya kosa lao.


Kuhani atafanya upatanisho mbele ya Yawe, kwa ajili ya huyo mutu aliyekosa bila kujua, naye atasamehewa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ