Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 4:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka kwa ajili ya zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 4:25
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Utatwaa sehemu ya damu na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu kwa kidole chako, na damu yote inayobaki utaimwanga chini ya mazabahu.


Ninyi hamujui bado? Hamujapata kusikia? Hamukuambiwa tangu mwanzo? Hamujafahamu mwanzo wa dunia?


Kisha atatoka na kwenda kwenye mazabahu inayokuwa mbele ya Yawe na kufanya ibada ya upatanisho. Atatwaa sehemu ya damu ya yule ngombe dume na ya yule mbuzi na kupakaa pembe za mazabahu pande zote.


Itakuwa hivyo kwa sababu uzima wa kiumbe uko katika damu. Nimewaagiza kutolea damu kwenye mazabahu kwa kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya roho zenu, kwa sababu damu inafanya upatanisho, nao uzima uko katika damu.


Kisha, sehemu ya damu atazipakaa kwenye pembe za mazabahu inayokuwa katika hema la mukutano mbele ya Yawe. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.


Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha beberu na kumuchinjia pahali wanapochinjia sadaka za kuteketezwa mbele ya Yawe. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi.


Kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka ya kuondoa zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu iliyobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu.


Kisha kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka kwa ajili ya zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu.


Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kufukizia ubani wenye harufu nzuri, mbele ya Yawe katika hema la mukutano. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.


Sehemu ya damu yake ataipakaa pembeni ya mazabahu na ile ingine ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi.


Kisha Musa akatwaa mafuta ya kupakaa, akaipakaa ile hema na vitu vyote vilivyokuwa ndani yake akavitakasa.


Musa akamuchinja huyo ngombe, akatwaa damu akapakaa pembe za mazabahu pande zote kwa kidole chake kwa kuitakasa. Kisha akatwaa damu iliyobaki akaimwanga chini kwenye tako la mazabahu ambayo alitakasa kwa kuifanyia ibada ya upatanisho.


Wana wake wakamuletea damu, naye akachovya kidole chake katika damu hiyo na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu. Damu iliyobakia akaimwanga kwenye tako la mazabahu.


Kwa maana kwa njia ya Kristo, Sheria imepata kufikia ukomo wake kusudi kila mutu anayeamini apate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.


Kwa hiyo ilifaa kwamba Mungu aliyeumba vitu vyote na kuvilinda imara, amufanye Yesu kuwa mukamilifu kwa njia ya mateso, kusudi awalete watoto wengi kuwa washiriki wa utukufu wa Mungu. Kwa maana Yesu ndiye anayewaongoza watu wapate kuokoka.


Na kufuatana na Sheria, karibu vitu vyote vinatakaswa kwa damu, nazo zambi haziwezi kusamehewa pasipo kumwangwa kwa damu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ