Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 4:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 mara tu akijulishwa zambi hiyo aliyotenda, ataleta sadaka yake ya beberu asiyekuwa na kilema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 4:23
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maovu yetu umeyaweka mbele yako; zambi zetu za siri ziko wazi mbele yako.


Kesho yake, utatoa beberu asiyekuwa na kilema, kuwa sadaka ya kusamehewa zambi; mazabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa damu ya ngombe dume.


Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;


Mutatoa beberu mumoja wa sadaka kwa ajili ya zambi na wana-kondoo dume wawili wa mwaka mumoja kwa ajili ya sadaka za amani.


mara tu zambi hiyo itakapojulikana, watatoa ngombe dume muchanga akuwe sadaka kwa ajili ya zambi. Watamuleta kwenye hema la mukutano.


Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha beberu na kumuchinjia pahali wanapochinjia sadaka za kuteketezwa mbele ya Yawe. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi.


mara tu atakapojulishwa kwamba ametenda zambi, ataleta sadaka ya mbuzi dike asiyekuwa na kilema kwa ajili ya zambi aliyotenda.


Ikiwa kuhani ambaye amepakwa mafuta ndiye aliyetenda zambi hata akawatia watu katika kosa, basi huyo atamutolea Yawe ngombe dume muchanga asiyekuwa na kilema akuwe sadaka kwa ajili ya zambi.


Au, kama mutu akiapa kufanya kitu chochote, chema au kibaya, kama vile watu wanavyofanya bila kufikiri, atakapojua atakuwa na kosa.


Uwaambie Waisraeli watwae beberu mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi, na mwana-ngombe mumoja na mwana-kondoo mumoja wote wa umri wa mwaka mumoja na wasiokuwa na kilema kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa,


basi, ikiwa kosa hilo limefanyika bila kukusudia, bila Waisraeli wote pamoja kujua, watatoa mwana-ngombe dume mumoja kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe, pamoja na sadaka yake ya vyakula na ya kinywaji kufuatana na maagizo yake. Vilevile watu watatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi.


Tena mutamutolea Yawe sadaka kwa ajili ya zambi, beberu mumoja, zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kila siku na sadaka yake ya kinywaji.


Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi kwa kuwafanyia upatanisho.


Mutatoa vilevile beberu mumoja kwa sadaka kwa ajili ya zambi zaidi ya sadaka ya kufanyiwa upatanisho, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya vyakula na sadaka zake za kinywaji.


Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.


Mutatoa vilevile beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi, zaidi ya sadaka ya kuteketezwa ya kawaida pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka yake ya kinywaji.


Tena mutatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi kwa kuwafanyia upatanisho.


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ