Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 4:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Kisha atamutwaa ngombe dume huyu na kumupeleka inje ya kambi na kumuteketeza kwa moto kama vile alivyofanya yule mwingine. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi ya jamii.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 4:21
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, watu wote waliorudi kutoka katika uhamisho wakamutolea Mungu wa Israeli sadaka zao za kuteketezwa kwa moto. Wakatoa ngombe dume kumi na wawili kwa ajili ya Israeli yote, kondoo dume makumi kenda na sita na wana-kondoo makumi saba na saba; vilevile walitoa mbuzi kumi na wawili kama sadaka ya kusamehewa zambi. Nyama wote hawa walitolewa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe.


Lakini nyama ya ngombe dume yule pamoja na ngozi na mavi yake utavitwaa na kuviteketeza inje ya kambi yenu. Hii itakuwa sadaka ya kuondoa zambi.


Siku hiyo, mufalme atatoa ngombe dume mumoja kwa ajili ya sadaka ya kusamehewa zambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa Israeli.


Halafu atachinja yule beberu wa sadaka ya zambi kwa ajili ya watu wote. Damu ya mbuzi huyo ataileta ndani ya Pahali Patakatifu Sana na kufanya kama vile alivyofanya na damu ya yule ngombe dume; atainyunyiza juu ya kiti cha rehema, upande wake wa mbele.


Haruni ataweka mikono yake juu ya kichwa cha huyo beberu muzima na kuungama juu yake zambi zote za watu wa Israeli, makosa yao yote na zambi zao zote; naye ataziweka zote juu ya kichwa cha yule mbuzi. Kisha atamwacha huyo beberu aende katika jangwa akipelekwa kule na mutu yeyote anayekuwa tayari.


Yule ngombe dume na mbuzi waliotolewa sadaka kwa ajili ya zambi ambao damu yao ilipelekwa katika Pahali Patakatifu kwa kufanya ibada ya upatanisho, watapelekwa inje ya kambi na kuteketezwa kwa moto. Ngozi zao, nyama na mavi yao, vyote vitateketezwa kwa moto.


Ikiwa Waisraeli wote pamoja wametenda zambi bila kukusudia kwa kufanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe,


Kwa hiyo atamufanya ngombe dume huyu kama alivyomufanya yule mwingine wa sadaka kwa ajili ya zambi. Basi, huyo kuhani atawafanyia watu ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi, nao watasamehewa.


Wazao wanaume wa Haruni ndio peke yao wanaoruhusiwa kula sehemu hiyo maana hiyo imetengwa siku zote kwa ajili yao kutoka sadaka Yawe anazotolewa kwa moto. Yeyote atakayezigusa atakuwa mutakatifu.


Lakini kama damu ya sadaka yoyote kwa ajili ya zambi imeletwa ndani ya hema la mukutano kwa kufanya ibada ya upatanisho katika Pahali Patakatifu, sadaka hiyo itateketezwa kwa moto.


Lakini nyama ya ngombe huyo, ngozi yake na mavi yake, akaviteketeza kwa moto inje ya kambi kama vile alivyoamuriwa na Yawe.


basi, ikiwa kosa hilo limefanyika bila kukusudia, bila Waisraeli wote pamoja kujua, watatoa mwana-ngombe dume mumoja kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe, pamoja na sadaka yake ya vyakula na ya kinywaji kufuatana na maagizo yake. Vilevile watu watatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi.


Kwa maana Mwana wa Mutu hakukuja kutumikiwa, lakini kutumikiana na kutoa maisha yake kusudi awakomboe watu wengi.”


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Kuhani Mukubwa anapeleka damu ya nyama ndani ya Pahali Patakatifu Sana kwa ajili ya kuitoa kuwa sadaka ya kusamehewa zambi lakini viungo vyote vya nyama wale vinateketezwa kwa moto mbali na kambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ