Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 4:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Kwa hiyo atamufanya ngombe dume huyu kama alivyomufanya yule mwingine wa sadaka kwa ajili ya zambi. Basi, huyo kuhani atawafanyia watu ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi, nao watasamehewa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 4:20
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kesho yake Musa akawaambia watu: Mumetenda zambi kubwa! Sasa nitamwendea Yawe juu kwenye mulima; labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya zambi yenu.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


ataweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama wa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, ambayo itakubaliwa kwa ajili ya kumufanyia huyo mutu upatanisho.


Kama hawezi kutoa mwana-kondoo, basi, ataleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa; mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya zambi. Kuhani atamufanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.


Yale mafuta yaliyobaki atayapakaa yule mutu kwenye kichwa. Hivyo kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho mbele ya Yawe.


Kuhani atatoa hao, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kuhani atamufanyia mutu huyu ibada ya upatanisho mbele ya Yawe na kumwondolea uchafu wake wa kutokwa na usaha.


Kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa kutumia kondoo huyo mbele ya Yawe kwa ajili ya zambi aliyotenda, naye atasamehewa zambi hiyo aliyotenda.


Kisha atamutwaa ngombe dume huyu na kumupeleka inje ya kambi na kumuteketeza kwa moto kama vile alivyofanya yule mwingine. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi ya jamii.


Mafuta yote ya beberu huyo atayateketeza juu ya mazabahu, kama vile anavyofanya na mafuta ya nyama wa sadaka ya amani. Kwa hiyo kuhani atamufanyia mutawala ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.


Kisha ataondoa mafuta yote kama vile anavyoondoa mafuta ya mwana-kondoo wa sadaka ya amani na kuhani atayateketeza juu ya mazabahu, pamoja na sadaka zinazotolewa kwa Yawe kwa moto. Kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.


Kisha ataondoa mafuta yote ya ngombe huyo: mafuta yanayofunika matumbotumbo,


Kisha atamutoa yule wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa kulingana na maagizo. Kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.


Basi, kuhani atamufanyia yule mutu ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi, naye atasamehewa. Unga unaobaki utakuwa wa kuhani kama vile inavyofanyika juu ya sadaka ya ngano.


Zaidi ya hayo, yule mutu atalipa hasara yote aliyosababisha juu ya vitu vitakatifu kwa kuongeza sehemu moja ya tano ya bei yake na kumupatia kuhani yote. Basi, kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi kwa huyo kondoo dume anayekuwa sadaka kwa ajili ya kosa, naye atasamehewa.


Atamuletea kuhani kondoo dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake ikiwa na bei sawa na ile ya sadaka ya kosa. Na kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa kosa alilofanya, naye atasamehewa.


na kumuletea Yawe sadaka yake kwa ajili ya kosa. Kwa ajili ya zambi aliyotenda ataleta kondoo dike au mbuzi dike kutoka kundi lake amutoe sadaka kwa ajili ya zambi. Naye kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake.


Hii ndio sheria juu ya ibada inayoelekea sadaka ya vyakula. Wazao wa Haruni ndio wanaokuwa na uwezo wa kumutolea Yawe sadaka hiyo juu ya mazabahu.


Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya Waisraeli wote pamoja, nao watasamehewa kwa sababu si kosa lililokusudiwa, na wameleta sadaka yao, sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe kama sadaka ya zambi kwa ajili ya kosa lao.


Kuhani atafanya upatanisho mbele ya Yawe, kwa ajili ya huyo mutu aliyekosa bila kujua, naye atasamehewa.


Wala si ile tu, lakini tunafurahi kwa ajili ya Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo aliyetupatanisha sasa na Mungu.


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.


Kwa hiyo ilimupasa afanane na wandugu zake katika mambo yote, kusudi apate kuwa Kuhani Mukubwa anayekuwa mwenye huruma na mwaminifu katika kazi yake mbele ya Mungu, na kwa njia hiyo zambi za watu zisamehewe.


Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.


Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.


Yeye ndiye sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu, wala si kwa ajili ya zambi zetu tu, lakini kwa ajili ya zambi za watu wote.


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ