Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kisha, kutoka katika sadaka hiyo ya amani Yawe anayotolewa kwa moto, atamutolea sehemu hizi: mafuta yake, mukia muzima wenye mafuta uliokatwa karibu kabisa na uti wa mugongo pamoja na mafuta yote yanayofunika matumbotumbo na mafuta yote yanayokuwa kwenye matumbotumbo,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 3:9
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha waliliingiza Sanduku la Yawe ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha pale na kuliweka pahali pake. Naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele ya Yawe.


Solomono alipoamuka, alitambua kwamba ilikuwa ndoto. Halafu akarudi Yerusalema, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Yawe, akamutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Halafu akawafanyia watumishi wake wote karamu.


Naye Solomono alimutolea Yawe sadaka za amani: ngombe elfu makumi mbili na mbili na kondoo elfu mia moja na makumi mbili. Hivi ndivyo mufalme na watu wote wa Israeli walivyozindua nyumba ya Yawe.


Siku hiyohiyo, mufalme aliizindua sehemu ya katikati ya uwanja uliokuwa mbele ya nyumba ya Yawe, maana ni pale ndipo alipotolea sadaka za kuteketezwa, sadaka za ngano, na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu ile mazabahu ya shaba haikutosha kwa sadaka hizo zote.


Kisha wakaingiza Sanduku la Agano, na kuliweka ndani ya hema ambayo Daudi alikuwa ametayarisha. Halafu wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto na za amani mbele ya Mungu.


Kisha utatwaa mafuta ya yule kondoo dume: mukia wake, mafuta yanayofunika matumbotumbo na sehemu bora ya maini, figo zake mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kuume. (Kondoo yule ni kondoo wa utakaso.)


Mwana wangu, unisikilize kwa uangalifu, ufuate mwenendo wa maisha yangu.


Yawe alipenda kumuponda kwa mateso. Alitoa uzima wake kwa ajili ya kuondoa zambi. Mutumishi wa Mungu atakuwa na wazao; ataishi maisha marefu. Yeye ndiye atakayetimiza mupango wa Yawe.


Agizo hili linalazimisha Waisraeli kuletea Yawe nyama ambao wanawachinja katika mashamba. Wataleta nyama wale kwa kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano, naye atawachinja na kumutolea Yawe sadaka za amani.


Mafuta yake yote: mafuta ya mukia na yale yanayofunika matumbotumbo yatatolewa na kuteketezwa


Kisha, akatwaa mafuta yote, mukia pamoja na mafuta yake, mafuta yote yanayofunika matumbotumbo, sehemu bora ya maini, pamoja na figo zote mbili, mafuta yake na paja la muguu wa kuume wa nyuma wa huyo kondoo dume.


Mafuta ya ngombe dume huyo na kondoo dume, mukia wa kondoo, mafuta yaliyofunika matumbotumbo, figo na sehemu bora ya maini


na kwa ajili ya sadaka ya amani, jumla ya nyama waliotolewa ilikuwa ngombe dume makumi mbili na wane, kondoo dume makumi sita, beberu makumi sita, na wana-kondoo dume wa mwaka mumoja makumi sita. Hiyo ndiyo iliyokuwa sadaka iliyotolewa kwa ajili ya mazabahu, kisha mazabahu hayo kupakwa mafuta.


Utanitangulia kwenda Gilgali, pahali ambapo nitakukuta na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani. Utaningojea pale kwa muda wa siku saba mpaka nikuje na kukuonyesha la kufanya.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ