Walawi 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
8 akiweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja mbele ya hema la mukutano. Makuhani wazao wa Haruni watanyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.
Kisha, atamuchinja huyo ngombe mbele ya Yawe. Nao makuhani wazao wa Haruni wataichukua damu na kuinyunyizia mazabahu inayokuwa kwenye mulango wa hema la mukutano, pande zake zote.
akiweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja mbele ya hema la mukutano. Wazao wa Haruni watanyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.
Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha beberu na kumuchinjia pahali wanapochinjia sadaka za kuteketezwa mbele ya Yawe. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi.
Ataleta huyo ngombe dume muchanga kwenye mulango wa hema la mukutano, mbele ya Yawe. Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha ngombe dume huyo na kumuchinja mbele ya Yawe.
Ndiyo kusema, Mungu ndiye aliyekuwa akipatanisha watu wote na yeye mwenyewe kwa njia ya Kristo bila kuhesabu makosa yao. Yeye ametupatia ujumbe wa upatanisho.
Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.