akiweka mukono wake juu ya kichwa cha nyama huyo na kumuchinja mbele ya hema la mukutano. Wazao wa Haruni watanyunyizia mazabahu damu yake pande zake zote.
Mafuta yote ya mbuzi huyo atayaondoa kama vile anavyoondoa mafuta ya nyama wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya mazabahu, na harufu yake nzuri itamupendeza Yawe. Basi, kuhani atamufanyia yule mutu hiyo ibada ya upatanisho, naye atasamehewa.