Katika miji ya inchi yenye milima, katika miji ya Shefela na katika miji ya jangwa la Negebu, katika inchi ya Benjamina, kandokando ya Yerusalema na katika miji ya Yuda, watu watahesabu tena kondoo wao. –Ni Yawe anayesema.
Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.
Kuelekea Walawi, hao nimewapa sehemu ya kumi ya kila kitu Waisraeli wanachonitolea kuwa urizi wao. Haya yatakuwa malipo yao kwa kazi wanayotoa katika kulitunza hema la mukutano.