Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 27:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mwanaume wa miaka makumi mbili mpaka miaka makumi sita atakombolewa kwa feza shekeli makumi tano kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 27:3
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, nafasi za kuabudu miungu kwenye milima hazikuharibiwa, na watu waliendelea kutambika na kufukiza ubani kule.


Kila mumoja atakayehesabiwa anapaswa kulipa nusu ya shekeli kulingana na vipimo vya hema la mukutano. Hii ni sadaka yake atakayonitolea.


Zahabu yote waliyomutolea Yawe kwa ajili ya kujenga hema takatifu ilikuwa na uzito wa kilo mia nane makumi saba na saba na grama mia tatu kulingana na vipimo vya hema takatifu.


Mutu akitakasa nyumba yake kuwa takatifu kwa Yawe, kuhani ataamua bei yake kulingana na uzuri au ubaya wake. Jinsi atakavyoamua, ndivyo itakavyokuwa.


Kila bei itapimwa kwa kipimo cha uzito cha shekeli kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu: uzito wa gera makumi mbili ni sawa na uzito wa shekeli moja.


Kama ni mwanamuke, atakombolewa kwa feza shekeli makumi tatu.


Kama mutu yeyote akikosa kwa kutenda zambi bila kujua juu ya kutokutoa vitu vitakatifu Yawe anavyotolewa, atamuletea kondoo dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake. Wewe utapima bei yake kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya kosa.


Moto utaendelea kuwaka siku zote juu ya mazabahu bila kuzimika hata kidogo.


Wazaliwa hao wa kwanza watakombolewa wakiwa wenye umri wa mwezi mumoja kwa kulipiwa feza shekeli tano, kulingana na vipimo vya hema takatifu.


utapokea kwa kila mwanaume feza shekeli tano, kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu, ambayo ni sawa na gera makumi mbili,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ