Kama ni nyama muchafu, mwenyeji atamununua kwa kulingana na jinsi munavyomupima na ataongeza asili mia makumi mbili ya bei ya nyama huyo. Kama hakombolewi, basi atauzishwa kulingana na vipimo vyenu.
Lakini wazaliwa wa kwanza wa ngombe, kondoo au mbuzi wasikombolewe; hao ni watakatifu. Damu yao utainyunyizia mazabahu na mafuta yao utayateketeza kuwa sadaka ya kuteketezwa ambayo ni harufu nzuri inayonipendeza mimi Yawe.
maana kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri nilijitakasia kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli; kila muzaliwa wa kwanza wa mwanadamu hata wa nyama; wao watakuwa wangu. Mimi ni Yawe.
“Umutolee Yawe, Mungu wako, wazaliwa wote wa kwanza dume wa kundi lako la ngombe na kondoo. Usiwafanyizishe ngombe hao kazi na kondoo hao usiwakate manyoya.