Lakini ikiwa hana uwezo wa kulikomboa, basi, litabaki katika mikono ya yule aliyelinunua mpaka mwaka wa sikukuu ya ukumbusho wa miaka makumi tano. Katika mwaka huo, mali hiyo iachiliwe na kurudishiwa kwa yule mutu aliyeiuzisha.
kuhani ataamua bei ya shamba hilo kwa kulingana na miaka inayobaki kufikia mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano na mutu huyo atalipa bei yake kama ni kitu kitakatifu kwa Yawe.
Kila bei itapimwa kwa kipimo cha uzito cha shekeli kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu: uzito wa gera makumi mbili ni sawa na uzito wa shekeli moja.