Ikiwa mutu yeyote atashindwa kufika katika muda wa siku tatu, kulingana na amri iliyotolewa na viongozi, mali yake yote itanyanganywa, naye mwenyewe atatengwa mbali na makutano na jamii ya watu waliorudi kutoka katika uhamisho.
Mwaka wa makumi tano mutauheshimu kwa kutangaza uhuru kwa watumwa wote katika inchi. Mwaka huo utakuwa ni sikukuu ya ukumbusho wa miaka makumi tano. Kila mumoja wenu atarudilia mali yake na jamaa yake.
Lakini ikiwa hana uwezo wa kulikomboa, basi, litabaki katika mikono ya yule aliyelinunua mpaka mwaka wa sikukuu ya ukumbusho wa miaka makumi tano. Katika mwaka huo, mali hiyo iachiliwe na kurudishiwa kwa yule mutu aliyeiuzisha.
Lakini nyumba za vijiji ambavyo havikuzungushiwa ukuta zitakuwa chini ya sheria ileile ya mashamba. Nyumba hizo zinaweza kukombolewa katika mwaka mumoja lakini ni lazima zirudishwe kwa wenyeji katika mwaka wa kukumbuka miaka makumi tano.
Mutakusanya vitu vyote mulivyoteka katika kiwanja cha muji na kuchoma kwa moto vitu vile vyote kama vile sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yawe, Mungu wenu. Muji huo utakuwa lundo la mabomoko milele, nao hautajengwa tena.
Muji ule utaangamizwa na kila kitu kinachokuwa mule maana umetolewa kwa Yawe. Rahabu, yule kahaba, ndiye atakayeachwa pamoja na wale ambao wako ndani ya nyumba yake kwa sababu aliwaficha wapelelezi wetu.