20 Lakini kama hataki kulikomboa au amemwuzishia mutu mwingine, basi, shamba hilo lisikombolewe tena.
Kama mwenyeji akitaka kulikomboa, basi, aongeze asili mia makumi mbili ya bei ya shamba hilo, na kisha litakuwa mali yake.
Katika mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano shamba hilo litaachiliwa na kuwa la Yawe milele. Kuhani ndiye atakayelirizi.
Lakini katika mwaka wa ukumbusho wa miaka makuni tano, shamba hilo lirudishiwe yule mutu aliyeliuzisha.