Mwaka wa makumi tano mutauheshimu kwa kutangaza uhuru kwa watumwa wote katika inchi. Mwaka huo utakuwa ni sikukuu ya ukumbusho wa miaka makumi tano. Kila mumoja wenu atarudilia mali yake na jamaa yake.
Kwa sababu mwaka huo ni wa sikukuu ya ukumbusho wa miaka makumi tano, musipande mbegu au kuvuna chochote kinachoota chenyewe wala kuchuma zabibu kutoka miti musiyokata matawi.
Mutu akitakasa shamba lake, ambalo ni urizi wake, kwa ajili ya Yawe, basi, bei yake itapimwa kulingana na mbegu zinazotumiwa kwa kupanda shamba hilo. Kwa kila kilo makumi mbili za shayiri bei yake itakuwa shekeli makumi tano za feza.
Lakini kama akilitakasa kisha mwaka huo, basi, kuhani ataamua bei yake kulingana na miaka inayobaki kufikia mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano na bei yake ipunguzwe.