Kama mutu mwingine akikula chakula kitakatifu bila kujua, basi, atalipa nyongezo ya sehemu moja ya tano pamoja na kipimo sawasawa alichokula na kumurudishia kuhani.
Hairuhusiwi kumubadilisha nyama huyo na mwingine yeyote, muzuri kwa mubaya au mubaya kwa muzuri. Kama akimubadilisha na nyama mwingine, wote wawili watakuwa watakatifu.
Kama ni nyama muchafu, mwenyeji atamununua kwa kulingana na jinsi munavyomupima na ataongeza asili mia makumi mbili ya bei ya nyama huyo. Kama hakombolewi, basi atauzishwa kulingana na vipimo vyenu.
Zaidi ya hayo, yule mutu atalipa hasara yote aliyosababisha juu ya vitu vitakatifu kwa kuongeza sehemu moja ya tano ya bei yake na kumupatia kuhani yote. Basi, kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi kwa huyo kondoo dume anayekuwa sadaka kwa ajili ya kosa, naye atasamehewa.