Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Nitawarehemu na kuwajalia mupate watoto wengi na kuongezeka. Nami nitaliimarisha agano langu nanyi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:9
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akawabariki na kuwaambia: “Muzae, muongezeke, na mujaze inchi na kuitawala. Mutawale samaki wa bahari, ndege wa anga, na kila kiumbe chenye uzima kinachotembea katika dunia.”


“Na juu ya Isimaeli, nimesikia ombi lako. Nitamubariki, nitamujalia watoto wengi na kuwazidisha sana. Isimaeli atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, nami nitamufanya kuwa baba wa taifa kubwa.


hakika nitakubariki, na wazao wako nitawazidisha kama nyota mbinguni na kama muchanga pembeni ya bahari. Wazao wako watarizi miji ya waadui zao.


Nitawazidisha wazao wako wakuwe kama nyota za mbinguni na kuwapa inchi hizi zote. Kutokana na wazao wako, mataifa yote katika dunia yatabarikiwa,


Wazao wako watakuwa wengi kama mavumbi ya dunia, na urizi wao utaenea kila pahali: upande wa magaribi, mashariki, kaskazini na kusini. Kwa njia yako na ya wazao wako, jamaa zote katika dunia zitabarikiwa.


Mungu Mwenye Nguvu akubariki upate wazao wengi na kuongezeka, kusudi ukuwe jamii kubwa ya watu.


Akaniambia: ‘Nitakufanya ukuwe na wazao na uongezeke. Nitakufanya ukuwe babu ya jamii kubwa za watu. Inchi hii nitawapa wazao wako, wairizi milele.’ ”


Lakini nitafanya agano nawe. Utaingia katika chombo, wewe pamoja na muke wako, wana wako na wake zao.


Na hapa umeniweka kati ya watu wako ambao umewachagua; nao ni wengi hata hawawezi kuhesabika kwa sababu ya wingi wao.


Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.


Nikawajibu: “Mungu wa mbinguni atatufanikisha katika kazi hii, nasi tunaokuwa watumishi wake tutaanza kujenga. Lakini ninyi hamuna sehemu au haki wala ukumbusho katika Yerusalema.”


Ukafanya wazao wao kuwa wengi kama nyota za mbinguni; ukawaleta katika inchi uliyowaahidi babu zao.


Aliwabariki watu wake, wakaongezeka; na hesabu ya wanyama wao akaizidisha.


Nitasema kwamba wema wako unadumu kwa milele, uaminifu wako ni imara kama mbingu.


Lakini wazao wa Israeli wakaongezeka sana, wakakuwa wengi na wenye nguvu sana, wakaenea kila pahali katika inchi ya Misri.


Mungu akawaangalia Waisraeli, naye akatambua hali yao.


Tena nilifanya agano nao kwamba nitawapa inchi ya Kanana ambako waliishi kama wageni.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Kisha, nitawakusanya kondoo wangu waliobaki kutoka inchi zote nilipowafukuza, na kuwarudisha katika malisho yao. Nao watazaa na kuongezeka.


Nitawapa wachungaji watakaowatunza vema, nao hawatakuwa na woga tena wala kufazaika, na hakuna hata mumoja wao atakayepotea. –Ni ujumbe wa Yawe.


Uniite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichwa ambayo haujapata kuyajua.


Mimi nitafanya agano nawe, nawe utatambua kwamba mimi ni Yawe.


Mimi niko upande wenu, nitahakikisha kuwa udongo wenu utalimwa na kupandwa mbegu.


kama mukizarau masharti yangu na kuchukia kwa roho maagizo yangu mukiacha kutii amri zangu zote na kuvunja agano langu,


Aliahidi kuwasikilia babu zetu huruma; na kukumbuka agano lake takatifu,


Yawe atawafanikisha kwa wingi: watoto, mifugo na mavuno katika shamba katika inchi aliyowaapia wazee wenu kwamba atawapa.


“Mutabarikiwa mupate wazao wengi, mavuno mengi, ngombe na kondoo wengi.


Atawapenda na kuwabariki, nanyi mutaongezeka na kuwa na wazao wengi. Atabariki mashamba yenu kusudi mupate ngano, divai na mafuta. Atawabariki kwa kuwapa ngombe na kondoo wengi katika inchi aliyowaahidi babu zenu kwamba atawapa ninyi.


Agano lile halitakuwa sawa na lile nililofanya na babu zao siku nilipowakamatia kwenye mukono na kuwaondoa toka inchi ya Misri. Kwa sababu hawakushika lile agano, kwa hiyo vilevile sikuwashugulikia. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ