Mungu akawabariki na kuwaambia: “Muzae, muongezeke, na mujaze inchi na kuitawala. Mutawale samaki wa bahari, ndege wa anga, na kila kiumbe chenye uzima kinachotembea katika dunia.”
“Na juu ya Isimaeli, nimesikia ombi lako. Nitamubariki, nitamujalia watoto wengi na kuwazidisha sana. Isimaeli atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, nami nitamufanya kuwa baba wa taifa kubwa.
Wazao wako watakuwa wengi kama mavumbi ya dunia, na urizi wao utaenea kila pahali: upande wa magaribi, mashariki, kaskazini na kusini. Kwa njia yako na ya wazao wako, jamaa zote katika dunia zitabarikiwa.
Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.
Nikawajibu: “Mungu wa mbinguni atatufanikisha katika kazi hii, nasi tunaokuwa watumishi wake tutaanza kujenga. Lakini ninyi hamuna sehemu au haki wala ukumbusho katika Yerusalema.”
Atawapenda na kuwabariki, nanyi mutaongezeka na kuwa na wazao wengi. Atabariki mashamba yenu kusudi mupate ngano, divai na mafuta. Atawabariki kwa kuwapa ngombe na kondoo wengi katika inchi aliyowaahidi babu zenu kwamba atawapa ninyi.
Agano lile halitakuwa sawa na lile nililofanya na babu zao siku nilipowakamatia kwenye mukono na kuwaondoa toka inchi ya Misri. Kwa sababu hawakushika lile agano, kwa hiyo vilevile sikuwashugulikia. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo.