Haya ndiyo majina ya mashujaa wale wa Daudi: Yasobeamu, wa ukoo wa Hakemoni, aliyekuwa kiongozi wa “Wale makumi tatu.” Yeye alipigana kwa mukuki wake akaua watu mia tatu kwa mara moja katika vita.
Abisai, ndugu ya Yoabu, alikuwa mukubwa wa mashujaa makumi tatu. Yeye alipigana kwa mukuki wake na watu mia tatu, akawaua, akajipatia jina kati ya wale mashujaa watatu.
Wayuda waliokuwa katika majimbo nao vilevile wakajitayarisha kuyalinda maisha yao. Wakaokolewa kutoka kwa waadui zao, wakawaua watu yapata elfu kumi na tano, lakini hawakunyanganya mali zao.
Siku hiyo, mimi Yawe nitawalinda wakaaji wa Yerusalema. Wanaokuwa wazaifu zaidi kati yao watakuwa na nguvu kama mufalme Daudi. Wazao wa Daudi watashika usukani kwa kuwaongoza watu wa Yuda kama Mungu, au kama malaika wa Yawe.
Lakini musimwasi tu Yawe, wala musiwaogope wenyeji wa inchi hiyo. Maana wao ni kama mboga tu kwetu. Kingo yao imekwisha kuondolewa kwao naye Yawe yuko pamoja nasi. Musiwaogope!
Mutu mumoja anaweza namna gani kuwashinda watu elfu moja, au watu wawili wanaweza namna gani kuwashinda watu elfu kumi, isipokuwa kama mulinzi wao amewatupa, Yawe amewaacha?