Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Nitawapa amani katika inchi hata muweze kulala bila kuogopeshwa na chochote. Nitaondoa nyama wakali katika inchi na inchi yenu haitapatwa na vita.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:6
43 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Elisha aligeuka, akawaangalia na kuwalaani kwa jina la Yawe. Dubu wawili wakatoka katika pori, wakawararua vijana makumi ine na wawili kati yao.


Hata hivyo, utapata mwana ambaye atatawala kwa amani kwa sababu nitamupa amani na waadui zake wote wa jirani. Jina lake litakuwa Solomono, kwa maana katika siku za utawala wake, atailetea inchi ya Israeli amani na utulivu.


Basi, Yosafati akatawala kwa amani, na Mungu akamupa amani pande zote.


Utalala bila kuogopeshwa na mutu; watu wengi watakuomba musaada.


Nawe utapatana na mawe ya shamba, na nyama wakali watakuwa na amani nawe.


Ngombe wetu wakuwe na afya na nguvu, kusitokwe mimba wala kukosa kuibeba. Kusikuwe tena kilio katika mitaa yetu.


Analeta amani katika eneo lako; anakushibisha kwa ngano safi kabisa.


Yawe awape watu wake nguvu! Yawe awabariki watu wake kwa amani!


Ninakulilia kwa sauti, ee Mungu, nawe unanisikiliza kutoka kwenye mulima wako mutakatifu.


Lakini mimi umenijalia furaha kubwa ndani ya moyo, kuliko ya hao wanaokuwa na divai na ngano kwa wingi.


Utuonyeshe wema wako, ee Yawe, utujalie wokovu wako.


Sitawaondoa watu wale katika mwaka mumoja, inchi isibakie tupu na nyama wa pori wasiongezeke sana na kuwazidia nguvu.


Unapolala, hautakuwa na hofu, utapata usingizi muzuri.


Yatakuongoza katika njia yako, yatakulinda wakati unapolala, yatakushauria unapoamuka.


Humo kutakuwa barabara kubwa, nayo itaitwa Njia Takatifu. Watu wachafu hawatapitia humo, lakini wale watu wa Mungu tu; wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,


humo hamutakuwa simba, nyama yeyote mukali hatapitia humo, hao hawatapatikana humo. Lakini waliokombolewa ndio watakaopita humo.


Mimi ninafanya mwangaza na kuumba giza; ninaleta uheri na kusababisha hasara. Mimi Yawe ninatenda vitu hivi vyote.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Usiogope ee Yakobo, mutumishi wangu, wala usifazaike, ee Israeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Maana nitakuokoa toka huko mbali unapokuwa, nitawaokoa wazao wako kutoka katika uhamisho. Utarudi na kuishi kwa amani, wala hakuna mutu atakayekuogopesha.


Ndiyo maana mutu ataweza kusema hivi: Niliamuka nikatambua kwamba usingizi wangu ulinifalia sana.


Tena nitatuma nyama wa pori katika inchi hiyo na kuwanyanganya watoto wao na kuifanya inchi hiyo kuwa ukiwa, hata hakuna mutu yeyote atakayeweza kupita katika inchi ile kwa sababu ya nyama wakali.


Tena nitaleta vita juu ya inchi ile na kuamuru waiangamize na kuua watu na nyama wanaokuwa ndani yake.


Lakini Bwana wetu Yawe anasema: Tena nitauazibu Yerusalema kwa mapigo yangu mane ya hukumu kali: vita, njaa, nyama wakali na ugonjwa mukali, nipate kuangamiza watu na nyama ndani yake!


Nitafanya nao agano la amani. Nitaondoa nyama wakali katika inchi, kusudi kondoo wangu wakae katika mbuga kwa usalama na kulala katika pori.


Miti inayokuwa katika mashamba itazaa matunda, udongo utatoa mazao kwa wingi, nao wataishi kwa salama katika inchi yao. Nitakapovunja nira zao za utumwa na kuwaokoa toka katika mikono ya hao waliowafanya kuwa watumwa halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nitakutumia njaa na nyama wakali ambao wataua watoto wako; magonjwa makali, mauaji, na vita itakuja kukuangamiza. Ni mimi, Yawe, ninayesema hivyo.


Siku hiyo, wewe utaniita “Mume wangu”, na sio tena “Bali wangu”. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nitafanya agano na nyama wa pori, ndege pamoja na vyote vinavyotambaa, kusudi wasikuumize. Nitaondoa upinde, upanga na silaha za vita katika inchi, na kukufanya uishi kwa usalama.


Kwa hiyo, mutafuata masharti yangu na kutimiza maagizo yangu, kusudi mupate kuendelea kuishi kwa usalama katika inchi.


Inchi itatoa mazao yake nanyi mutakula na kushiba na kuishi mule kwa usalama.


Nitaleta nyama wakali kati yenu ambao watawanyanganya watoto wenu na kula mifugo yenu na kupunguza hesabu yenu hata njia zenu zigeuke kama jangwa.


Nitawaletea upanga ambao utalipiza kisasi juu ya agano mulilovunja. Ninyi mutakimbilia katika miji yenu, lakini nitawaletea ugonjwa mukali na kuwatia katika mikono ya waadui zenu.


Mutafukuza waadui zenu na kuwaua kwa upanga.


Kila mutu atakaa kwa amani chini ya miti ya tini na mizabibu yake, bila kutishwa na mutu yeyote. –Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe wa majeshi.


Waisraeli watakaobaki hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo, wala kwao hakutapatikana mudanganyifu yeyote. Watapata chakula na kulala wala hakuna mutu atakayewaogopesha.


Nyumba mupya itakuwa yenye utukufu zaidi kuliko ile ya kwanza. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo! Kutoka hapa nitawapa watu wangu fanaka. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!


Ataondoa kabisa magari ya vita katika inchi ya Efuraimu, na farasi wa vita kutoka katika Yerusalema; pinde za vita zitatupwa mbali. Naye ataleta amani kati ya mataifa; utawala wake utaenea toka bahari mpaka bahari, toka muto Furati hata miisho ya dunia.


“Ninawaachia amani; ninawapa amani yangu. Siwapatii ninyi amani hii kama dunia inavyoitoa. Musifazaike wala musiogope.


Usiku, mbele ya kutimia kwa siku Herode aliyotaka kumusambisha mbele ya watu, Petro alikuwa amelala ndani ya chumba katikati ya waaskari wawili. Alikuwa amefungwa na minyororo miwili, nao walinzi walikuwa wakichunga mulango wa kifungo.


Sasa kufuatana na vile tumekwisha kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani, kunakuwa sasa amani kati yetu na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ