Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

40 Lakini kama wakitubu uovu wao na uovu wa wazee wao juu ya uasi waliotenda juu yangu na vilevile juu ya kupingana kwao nami,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:40
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

kama watakapokuwa kule katika uhamisho wakijifikiri ndani yao wenyewe na kukugeukia, kama katika ile inchi ya uhamisho wakikusihi na kusema ‘Tumetenda zambi; tumepotoka na kufanya maovu’,


vilevile wakati ule watakapokuwa katika inchi ya waadui zao, wakikugeukia kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote, na kama wakikuomba wakielekea inchi yao ambayo uliwapatia babu zao, wakielekea muji huu ambao uliuchagua na nyumba hii ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako,


Sasa, mutubu zambi zenu mbele ya Yawe, Mungu wa babu zenu, na kufanya yale yanayomupendeza. Mujitenge na wakaaji wa inchi hii na kuwaacha wake zenu wa kigeni.”


Ee Yawe, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki na umetuacha tubaki kama vile tunavyokuwa hivi leo. Tunaungama makosa yetu mbele yako, tukijua kwamba hakuna anayekuwa na haki yoyote ya kuja mbele yako kwa ajili ya makosa haya.”


nikisema: “Ee Mungu wangu, ninaona haya kubwa sana kukiinua kichwa changu mbele yako. Zambi zetu zimelundikana kupita hata vichwa vyetu; makosa yetu yanafika hata mbinguni.


Kisha niliitikia makosa yangu mbele yako, wala sikuficha uovu wangu. Nilisema kwamba nitaungama makosa yangu mbele ya Yawe. Nawe ukanisamehe zambi yangu.


Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.


Tunakubali uovu wetu, ee Yawe, tunakubali uovu wa babu zetu, maana, tumekukosea wewe.


Ona, ee Yawe, ninavyokuwa tabani. Roho yangu imechafuka, moyo wangu unaugua maana nimekuasi vibaya. Kule inje kumejaa mauaji, ndani nako ni kama kifo tu.


Mienendo na matendo yao vitakuhakikishia kwamba hasara niliyouletea muji huo sikuileta bila sababu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Kisha mutakapokumbuka mienendo yenu miovu na matendo yenu mabaya, mutajichukia wenyewe kwa sababu ya maovu yenu na machukizo muliyofanya.


Nitarudi mahali pangu na kujitenga nao mpaka watambue kosa lao na kunirudilia. Taabu zao zitawafundisha wanitafute.


Kama mukiendelea kunipinga na kukataa kunisikiliza, nitazidisha tena azabu yenu mara saba kadiri ya wingi wa zambi zenu.


basi, nami nitapingana nanyi na kuwaazibu mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


Basi, mutu akiwa na kosa juu ya mambo hayo lazima akubali zambi yake aliyotenda


Anapaswa kutubu zambi yake aliyotenda; na atatoa malipo kamilifu kwa kosa lake, akiongeza asilimia makumi mbili ya malipo hayo; atatoa malipo hayo kwa yule aliyemukosea.


Nao wakawaendea watu wa makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase kule Gileadi wakawaambia:


Yoshua akamwambia Akana: “Mwana wangu, umutukuze Yawe, Mungu wa Israeli, umusifu na kisha uniambie yale uliyotenda, wala usinifiche.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ