Yawe anasema hivi: ‘Angalia nitaleta uovu juu ya Yerusalema na juu ya wakaaji wake, laana zote zilizoandikwa katika kitabu kilichosomwa mbele ya mufalme wa Yuda.
Tangu nyakati za babu zetu mpaka sasa, sisi watu wako tumekukosea sana. Na kwa sababu ya zambi zetu, sisi, wafalme wetu na makuhani wetu tulitiwa katika mikono ya wafalme wa inchi za kigeni, tukauawa, tukapelekwa kuwa wafungwa na kunyanganywa mali zetu. Na hata hivi leo, tumetiwa haya kupita kiasi.
Lakini mukinirudilia, mukishika amri zangu na kuzifuata hata ingawa nitakuwa nimewatawanya mbali kabisa, nitawarudisha pahali nilipochagua kuwa pahali pangu pa kuabudiwa.’
Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.
Anawatendea mema maelfu, anawasamehe uovu, makosa na zambi. Lakini hataacha kumwazibu mwenye kosa. Anawalipiza watoto na wajukuu uovu wa baba na babu zao, hata kizazi cha tatu na cha ine.
Tunasikia nyimbo za sifa kutoka miisho ya dunia, nyimbo za kumusifu Mungu anayekuwa mwenye haki. Lakini mimi ninasema: Ninakonda, kweli ninakonda. Ole kwangu mimi! Wadanganyifu wanaendelea kuwa wadanganyifu, udanganyifu wao unazidi kuwa mubaya zaidi.
Sherti tujilaze chini kwa ajili ya haya, na kujiachilia kufunikiwa na haya yetu. Tangu ujana wetu mpaka leo hii, sisi wenyewe, kama vile babu zetu, tumetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wetu, wala hatukumutii Yawe, Mungu wetu.
Watu wa Yuda wamekwenda katika uhamisho, wakijaa mateso na kuwa katika utumwa mukali. Wanakaa kati ya watu wa mataifa, wala hawapati nafasi ya kupumzikia. Waliowafuatilia wamewakamata wakiwa katika taabu.
Lakini munauliza: Kwa nini mutoto asiazibiwe kwa sababu ya zambi za baba yake? Mutoto akitenda mambo ya haki na ya ukweli, kama akiwa mwangalifu kushika masharti yangu yote, basi, huyo hakika ataishi.
Ewe mwanadamu! Uwaambie Waisraeli jambo hili: Ninyi munasema: Tumezidiwa na makosa na zambi zetu. Tunaregea kwa sababu yake! Tutaweza namna gani kuishi?
Halafu wale walioponyoka watanikumbuka katikati ya mataifa ambamo watakuwa wamepelekwa katika uhamisho. Nitakuwa nimewavunja moyo wao wa uzinzi ambao ulinitupilia mbali, na macho yao yaliyozini na sanamu zao. Kwa hiyo watajichukia wao wenyewe kwa sababu ya maovu na machukizo yao yote waliyoyatenda.
“Mimi Yawe si mwepesi wa hasira, ni mwenye wema mwingi, na ni mwenye kusamehe uovu na makosa. Lakini kwa vyovyote vile sitakosa kuwaazibu watoto na wajukuu mpaka kizazi cha tatu na cha ine kwa zambi za wazazi wao.”
Hamutakuwa na raha yoyote pahali penu wenyewe pa kutulia wala kati ya mataifa hayo. Lakini Yawe atawapa huko wasiwasi wa moyo, kufifia kwa macho na mahangaiko ya ndani ya roho.
Musa akaendelea kusema: “Baraka na laana hizi zote zitatimizwa. Mutafikiri juu ya mambo hayo wakati Yawe, Mungu wenu, atakuwa amewatawanya kati ya mataifa.
Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.