Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Nitateketeza inchi yenu hivyo kwamba hata waadui wanaohamia mule watashangaa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:32
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na nyumba hii itaharibiwa na kuwa mabomoko. Kila mutu atakayepita karibu atashituka na kutikisa kichwa, na kuuliza: ‘Kwa nini Yawe amefanya hivyo kwa inchi hii na kwa nyumba hii?’


Sasa Yawe anaiharibu dunia na kuifanya tupu. Atavuruga uso wa dunia na kuwatawanya wakaaji wake.


Nitalifanya ukiwa kabisa, mizabibu yake haitasafishwa matawi wala kupaliliwa. Litaota michongoma na miiba. Tena nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.


Nimemusikia Yawe wa majeshi akisema hivi: Hakika nyumba nyingi zitabaki tupu, zile kubwa na nzuri zitabaki wazi bila wakaaji.


Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.


Nyumba yetu takatifu na nzuri, ambamo babu zetu walikusifu, imeteketezwa kwa moto. Pahali petu pote pazuri pamekuwa mabomoko.


Wamelifanya kuwa tupu; nalo linalilia katika ukiwa wake. Inchi yote imekuwa jangwa, wala hakuna mutu anayejali.


Wameifanya inchi yao kuwa kitisho, kuwa kitu cha kuzomewa siku zote. Kila mutu anayepita huko anashangaa na kutikisa kichwa chake.


Nitaufanya muji huu kuwa pahali pa kushangaza; nitaufanya kuwa kitu cha kuzomewa. Kila mutu anayepita karibu nao atashangaa na kuuzomea kwa sababu ya hasara zote zitakazowapata.


Inchi hii yote itakuwa katika mabomoko matupu na ukiwa, na mataifa jirani yatamutumikia mufalme wa Babeli kwa muda wa miaka makumi saba.


Kwanza nikakunywesha wakaaji wa Yerusalema na miji mingine ya Yuda, wafalme wake na wakubwa wa serikali yake kusudi ikuwe jangwa, ukiwa, kitu cha kuzomewa na cha kulaaniwa, kama inavyokuwa mpaka leo. Halafu nikakunywesha:


Yawe amewaacha watu wake, kama vile simba anavyoacha pango lake; inchi yao imekuwa jangwa tupu, kwa sababu ya vita na hasira kali ya Yawe.


Yawe anasema hivi: Katika muji huu ambao munasema kwamba umekuwa ukiwa bila watu wala nyama, katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema ambazo ni tupu, bila watu wala nyama, humo kutasikilika tena sauti za vicheko, sauti za furaha,


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninyi mumeona hasara yote niliyouletea Yerusalema na miji yote ya Yuda. Miji hii ni mabomoko mpaka leo wala hakuna mutu anayeishi humo.


Yawe hakuweza kuvumilia tena matendo yenu maovu na mambo ya kuchukiza muliyotenda; ndiyo maana inchi yenu imekuwa ukiwa, jangwa, laana na bila wakaaji, kama inavyokuwa mpaka leo.


Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?


Wafalme katika dunia hawakuamini wala wakaaji wowote wa ulimwengu, kwamba mwangamizaji na adui wangeweza kuingia katika milango ya Yerusalema.


Maana mulima Sayuni umeachwa utupu, mbweha wanazungukazunguka humo.


Utakuwa kitu cha kuzarauliwa na cha haya, mufano wa kitu cha kuchukiza kwa makabila yanayokuzunguka, wakati nitakapotimiza hukumu zangu juu yako kwa hasira na kasirani yangu kali. Ni mimi Yawe ninayasema hivyo.


Tega sikio, ee Mungu wangu; angalia uone taabu tunazokuwa nazo na jinsi huo muji unaoitwa kwa jina lako unavyotaabika. Tunakutolea maombi yetu si kwa sababu tumetenda haki, lakini kwa sababu wewe una huruma nyingi.


mimi Danieli nilikuwa nikisoma kwa uangalifu vitabu vitakatifu, na humo nikaelewa maana ya jambo lile Yawe alilomufahamisha nabii Yeremia juu ya ile miaka makumi saba, muda ambao utahusika na kuharibiwa kwa Yerusalema.


Hata kama miti ya tini isipochanua maua wala mizabibu kuzaa zabibu, hata kama mizeituni isipozaa zeituni na mashamba yasipotoa chakula, hata kama kondoo wakitoweka katika zizi na nyama wa kufugwa kukosekana katika mazizi,


“Wakati mutakapoona muji wa Yerusalema umezungukwa na waaskari, mujue kwamba uharibifu wake unakaribia.


Nanyi mutakuwa kinyaa, mazarau na mushangao kati ya watu wote wa inchi ambako Yawe atawapeleka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ