Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Nitaharibu pahali penu pa ibada kule juu ya milima, nitabomoa mazabahu zenu za kufukizia ubani, na kutupa maiti zenu juu ya sanamu za miungu yenu. Roho yangu itawachukia kabisa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:30
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

kwa maana kilio kilichomufikia Yawe juu ya wakaaji wa hapa ni kikubwa sana, naye ametutuma tukuje kuwaangamiza.”


Mutu huyo akailaani ile mazabahu akisema: “Ee mazabahu, Yawe anasema hivi: ‘Kutazaliwa mutoto katika ukoo wa Daudi, jina lake Yosia. Huyo atawatwaa makuhani wanaotumika kwa nafasi ya ibada na kufukiza ubani juu yako, na kuwatambika juu yako. Hakika, mifupa ya watu itateketezwa juu yako!’ ”


Mambo yote aliyoagizwa na Yawe juu ya mazabahu ya Beteli, na nafasi yote ya kutambikia juu ya vilima vya Samaria, hakika yatatimia.”


Kisha Yosia alipogeuka akaona makaburi juu ya kilima. Aliagiza mifupa ifukuliwe kutoka makaburi na kuichoma juu ya mazabahu. Basi akachafua mazabahu sawasawa na neno la Yawe ambalo mutu wa Mungu alilitangaza, nabii ambaye alitabiri matukio haya.


Aliwaua makuhani wote wa miungu ya uongo juu ya mazabahu ambapo walitumikia na kuchoma mifupa yao juu ya mazabahu hayo. Kisha akarudi Yerusalema.


Akakusanya makuhani wote kutoka miji ya Yuda na aliharibu pahali pa kuabudia makuhani walipofukiza ubani, kutoka Geba mpaka Beri-Seba. Akabomoa pahali pa kuabudia palipokuwa upande wa kushoto wa mulango wa muji kwenye milango iliyokuwa kwenye njia ya kuingilia kwenye mulango wa Yoshua mutawala wa muji.


Halafu watu wote wakaenda kwenye nyumba ya Bali na kuibomoa wakavunja mazabahu pamoja na sanamu zake, hata wakamwua Matani, kuhani wa Bali, mbele ya mazabahu.


Nyuma ya sherehe kumalizika, watu wote wa Israeli wakakwenda katika kila muji wa Yuda, wakavunjavunja nguzo za mawe na kukatakata sanamu za Ashera, mungu wa kike, na vilevile wakaharibu mazabahu na pahali pa kuabudia miungu mingine. Wakafanya vile katika inchi yote ya Yuda, Benjamina, Efuraimu na Manase, mpaka walipokwisha kuvimaliza vyote. Kisha Waisraeli wakarudi kwao, kila mutu kwenye urizi wake.


Hasira ya Yawe ikawawakia watu wake, akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake.


Utadumu milele kama mwezi unaokuwa mushuhuda mwaminifu asiyetoka katika anga.”


Hivi ndivyo uovu wa wazao wa Yakobo utakavyoondolewa, hivi ndivyo zambi yake itakavyofutwa kabisa: ataziharibu mazabahu za miungu; mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa. Sanamu za Ashera wala mazabahu za kufukizia ubani hazitabaki.


Ee Yawe, umekataa Yuda kabisa? Moyo wako umechukizwa na Sayuni? Kwa nini umetupiga vibaya kama hivi, hata hatuwezi kupona tena? Tulitazamia kupata amani, lakini hakuna kitu kizuri. Tulitazamia kupona, lakini tumepatwa na vitisho.


Nitalipiza kisasi mara mbili zaidi juu ya zambi zao na makosa yao, kwa sababu wameichafua inchi yangu na mizoga ya miungu yao yenye kuchukiza, wameijaza inchi yangu na hayo machukizo yao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitakutia katika mikono ya wapenzi wako, nao watabomoa nafasi yako yenye kuinuka na pahali pako pa kutambikia. Watakutosha nguo yako na kukunyanganya vitu vyako vya kujipamba, wakuache uchi, bila kitu.


naye akaniambia: Wewe mwanadamu! Hapa ndipo pahali pa kiti changu cha kifalme, pahali ninapoweka miguu yangu. Nitakaa kati ya watu wa Israeli milele. Na Waisraeli hawatalichafua jina langu, wao wenyewe, wala wafalme wao kwa kuziabudu sanamu au kuzika maiti za wafalme wao pahali hapa.


Wakati maiti zao zitakapokuwa zimelala kati ya sanamu zao za miungu, na kwenye mazabahu zao juu ya kila mulima, chini ya kila muti wenye kivuli, chini ya kila muti wa mwalo wenye majani na popote walipotolea sadaka zenye harufu nzuri ya kuzipendeza sanamu zao za miungu. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Mioyo yao imejaa udanganyifu. Sasa ni lazima wabebe makosa yao. Yawe atabomoa mazabahu zao na kuziharibu nguzo zao.


Musifuate desturi za taifa ninalofukuza mbele yenu. Maana waliyafanya hayo yote, nami nikawachukia sana.


Nitaweka makao yangu kati yenu, wala sitawaachilia.


kama mukizarau masharti yangu na kuchukia kwa roho maagizo yangu mukiacha kutii amri zangu zote na kuvunja agano langu,


Bwana wetu Yawe ameapa kwa nafsi yake: Ninachukizwa sana na kiburi cha wazao wa Yakobo; tena ninachukia nyumba zao nzuri sana. –Ni ujumbe wa Yawe.– Muji wao na vyote vinavyokuwa ndani yake nitavipatia waadui zake.


Kule kwenye vilima ambapo wazao wa Isaka wanatambikia, kutafanywa kuwa uharibifu mutupu na mahekalu ya Waisraeli yatakuwa mabomoko. Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mufalme Yeroboamu.


Yawe aliona jambo hilo akawaacha; aliwakataa watoto wake, wanaume na wanawake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ