Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Chakula chenu nitakipunguza hata wanawake kumi watumie mafika moja tu kwa kupika mikate. Watawagawanyia mukate wenu kwa kipimo. Na hata kisha kula mutaendelea kuwa na njaa tu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:26
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Matokeo yake ilikuwa njaa kali katika muji wa Samaria. Kichwa cha punda kilinunuliwa kwa vikoroti makumi tatu vya feza, na grama mia moja za mavi ya njiwa zilinunuliwa kwa vikoroti vitano vya feza.


Mungu alileta njaa katika inchi yao, akafunga njia zao zote za kupata chakula.


Sasa, Bwana wetu Yawe wa majeshi ataondoa kutoka Yerusalema na inchi ya Yuda kila tegemeo: tegemeo lote la chakula na la kinywaji.


Shamba la mizabibu lenye hektari kumi litatoa litre makumi tano tu za divai; anayepanda kilo mia moja za mbegu atavuna kilo kumi tu.


wananyanganya upande mumoja na hawatosheki; wanakula upande mwingine lakini hawashibi. Kila mumoja anamushambulia mwenzake.


Manase anashambulia Efuraimu, Efuraimu anashambulia Manase na wote wawili wanashambulia Yuda. Hata hivyo, hasira ya Yawe haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Hata wakifunga, sitayasikiliza maombi yao, na hata wakinitolea sadaka za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, mimi sitazikubali. Lakini nitawaangamiza kwa vita, njaa na ugonjwa mukali.


Wewe mwanadamu! Taifa fulani likitenda zambi kwa kukosa uaminifu kwangu, mimi nitanyoosha mukono wangu kwa kuliazibu. Nitaiharibu akiba yake ya chakula na kuliletea njaa. Nitawaua watu na nyama wake.


Chakula utakachokula kitapimwa, nacho kitakuwa grama mia mbili makumi tatu kwa siku; nawe utakula mara moja tu kwa siku.


Tena akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, mimi nitaharibu akiba ya chakula katika Yerusalema; wakaaji wake watakula chakula watakachopimiwa kwa hofu. Watakunywa maji watakayopimiwa kwa kufazaika.


Nitafanya hivyo kusudi wakose chakula na maji, na kila mumoja atamwangalia mwenzake kwa kufazaika; nao watakuwa zaifu kwa ajili ya azabu yao.


Wakati huo nitaiachilia mishale yangu mikali ya njaa iwachome na kuangamiza wakaaji wako. Nitawafanya wakufe na njaa kwa kuiharibu akiba yao ya chakula.


Watakula, lakini hawatashiba, watazini, lakini hawatapata watoto, kwa sababu wameniacha mimi Yawe, na kufuata miungu mingine.


Na kama hata kisha hayo yote bado hamutanisikiliza mukiendelea kunipinga,


Mutakula lakini hamutashiba; njaa itazidi kuwa katika tumbo yenu. Mukiweka akiba haitachungwa, na mukichunga kitu nitakiharibu kwa vita.


Munapanda mbegu kwa wingi, lakini munavuna kidogo. Munakula, lakini hamushibi. Munakunywa divai, lakini hamutosheki. Munavaa nguo, lakini bado munasikia baridi. Mushahara wa mutumishi unakuwa kama umetumbukizwa katika mufuko uliotoboka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ