Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Nitawaletea upanga ambao utalipiza kisasi juu ya agano mulilovunja. Ninyi mutakimbilia katika miji yenu, lakini nitawaletea ugonjwa mukali na kuwatia katika mikono ya waadui zenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:25
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yawe akawaletea Waisraeli ugonjwa, tangu asubui mpaka wakati uliopangwa. Watu elfu makumi saba walikufa katika inchi yote kutoka Dani mpaka Beri-Seba.


“Ikiwa watu wako Waisraeli wameshindwa na waadui zao kwa sababu ya zambi walizotenda mbele yako, nao wakikugeukia na kusifu jina lako, wakiomba na kukusihi katika nyumba hii,


“Ikiwa kuna njaa katika inchi, au ugonjwa mukali, ukosefu wa mvua, ugonjwa wa mimea, nzige au vidudu vingine, au ikiwa watu wako wameshambuliwa na waadui zao katika muji wao wowote, ikiwa kuna pigo lolote au ugonjwa wowote,


Mufalme Salmanaseri wa Asuria alimushambulia; naye Hoshea akakuwa mutumishi wake na kumulipa kodi.


Ingawa jeshi la Suria lilikuwa dogo, Yawe alilipatia ushindi mbele ya jeshi kubwa la watu wa Yuda kwa sababu hao watu wa Yuda walikuwa wamemwacha Yawe, Mungu wa babu zao. Hivi, Wasuria wakatimiza azabu ya Mungu juu ya mufalme Yoasi.


Ee Yawe, Mungu mwenye kulipiza kisasi, ewe Mungu mwenye kulipiza kisasi, ujitokeze!


Musa na Haruni wakamwambia: “Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Tunakusihi utuache tujiendee katika jangwa mwendo wa siku tatu tutoe sadaka kwa Yawe, Mungu wetu. Kama sivyo, yeye atatuua kwa ugonjwa mukali au kwa upanga.”


Lakini mukikataa na kuniasi, mutaangamizwa kwa upanga. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Nimewapangia kifo kwa upanga, ninyi wote mutanaswa kwa kuchinjwa! Maana, nilipowaita, hamukuniitikia; niliposema, hamukunisikiliza. Mulitenda maovu mbele yangu, mukachagua yale nisiyoyapenda.


Vilevile kwa nafasi hii nitaivuruga mipango ya watu wa Yuda na ya watu wa Yerusalema. Nitawatoa washindwe na kuuawa kwa panga na waadui zao, wale wanaovizia maisha yao. Nazo maiti zao nitaziacha kuwa chakula cha ndege na nyama wa pori.


Na zaidi ya ile nitawaletea vita, njaa na magonjwa makali mpaka waangamizwe kabisa kutoka katika inchi niliyowapa wao na babu zao.


Sikiliza! Wakimbizi na wenye kutoroka kutoka inchi ya Babeli wanakuja kutangaza huko Sayuni jinsi Yawe, Mungu wetu, alivyolipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake.


Yawe amezichochea roho za wafalme wa Wamedi, kwa maana amekusudia kuiangamiza Babeli. Kweli, hicho ndicho kisasi cha Yawe; analipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake. Munoe mishale yenu! Mutwae ngao!


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mufikiri na kuwaita wanawake waombolezaji; muwaite wanawake wanaoelewa nyimbo za kilio.


Maiti za vijana na wazee zimelala ndani ya mavumbi katika barabara, wabinti na vijana wangu wameuawa kwa upanga; umewaua bila huruma siku ya hasira yako.


Tena nitaleta vita juu ya inchi ile na kuamuru waiangamize na kuua watu na nyama wanaokuwa ndani yake.


Nitawalazimisha mukuwe chini ya uchungaji wangu kila mumoja, na kuwaongoza mupate kutii agano langu.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaleta upanga juu yako na kuwaua watu na nyama wako wote.


Wewe mwanadamu! Ongea na wanainchi wenzako, uwaambie hivi: Kama nikileta vita katika inchi fulani, na watu wa inchi hiyo wakimuchagua mumoja wao akuwe mulinzi wao,


Nitakutumia njaa na nyama wakali ambao wataua watoto wako; magonjwa makali, mauaji, na vita itakuja kukuangamiza. Ni mimi, Yawe, ninayesema hivyo.


na kusema hivi: Musikilize neno la Bwana wetu Yawe, enyi wakaaji wa milima ya Israeli! Anawaambia ninyi wakaaji wenye kuwa katika milima na vilima na katika maporomoko na mabonde kwamba: Mimi mwenyewe, Bwana wenu Yawe, nitaleta upanga na kuharibu sehemu zenu zote zilizoinuka za kutambikia.


Upanga utavuma katika miji yao, utavunjavunja miimo ya milango yake na kuwaangamiza katika kuta zao.


Nitawapa amani katika inchi hata muweze kulala bila kuogopeshwa na chochote. Nitaondoa nyama wakali katika inchi na inchi yenu haitapatwa na vita.


Niliwaletea ugonjwa mukali kama ule nilioupelekea Misri. Niliwaua vijana wenu katika vita, nikatwaa farasi wenu wa vita. Maiti zilijaa katika kambi zenu, harufu yake mbaya ikajaa katika pua zenu. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Ugonjwa mukali unatangulia mbele yake, nyuma yake hasara inafuata.


Nitawapiga kwa ugonjwa mukali na kuwatupilia mbali; lakini, kutokana nawe, nitaunda taifa lingine kubwa, lenye nguvu kuliko wao.


Basi Musa akazungumuza na watu akawaambia: Mutayarishe watu kwa vita waende kuwashambulia Wamidiani kwa kumulipizia Yawe kisasi.


Kutakuwa tetemeko kubwa la inchi. Vilevile kutakuwa njaa na magonjwa makali kwenye nafasi mbalimbali. Zaidi ya ile kutakuwa mambo ya kuogopesha na vitambulisho vya ajabu toka mbinguni.


Atawaletea ugonjwa mukali mpaka ninyi wote muangamie kabisa katika inchi ambayo munaenda kurizi.


Vita itasababisha vifo vingi inje, na ndani ya nyumba hofu itawatawala. Vijana wanaume na wanawake watauawa, hata wenye kunyonya na wazee wenye imvi.


Ni kazi yangu kulipiza kisasi, mimi nitalipiza, wakati miguu yao itakapoteleza; maana siku yao ya hasara imefika mwisho wao uko karibu sana.


nitanoa upanga wangu unaometemeta, nitanyoosha mukono kutoa hukumu, nitawalipiza kisasi waadui zangu, nitawaazibu wale wanaonichukia.


Basi, watu elfu tatu wa Yuda wakamwendea Samusoni katika pango chini ya jiwe la Etamu wakamwambia: “Haujui kwamba Wafilistini wanatawala juu yetu? Angalia basi, jambo ulilotutendea!” Samusoni akawajibu: “Kama walivyonitendea ndivyo nilivyowatendea.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ