Katika siku zile, hakuna mutu aliyeweza kuingia wala kutoka kwa usalama kwa sababu hapakukuwa amani; fujo nyingi sana ziliwasumbua wanainchi wa kila inchi.
Kwa sababu hiyo laana inaiteketeza dunia, wakaaji wake wanateseka kwa ajili ya makosa yao. Wakaaji wa dunia wamepunguka, ni watu wachache tu waliobaki.
Barabara kubwa zimebaki tupu; hakuna anayesafiri kupitia ndani yao. Mapatano yanavunjwa ovyo, washuhuda wanazarauliwa. Hakuna anayejali tena maisha ya wanadamu.
wakamwendea Yeremia, wakamwambia: Tafazali sikiliza maombi yetu na kutuombea kwa Yawe, Mungu wako, sisi wote tuliobaki, kwa maana tulikuwa wengi, lakini sasa tumebaki wachache tu, kama unavyoona.
Barabara za Sayuni zinaomboleza, maana hakuna anayepita kwa sikukuu. Milango yake yote ni tupu, makuhani wake wanaugua, wabinti zake wana huzuni, na muji wenyewe uko katika uchungu.
Tena nitatuma nyama wa pori katika inchi hiyo na kuwanyanganya watoto wao na kuifanya inchi hiyo kuwa ukiwa, hata hakuna mutu yeyote atakayeweza kupita katika inchi ile kwa sababu ya nyama wakali.
Lakini Bwana wetu Yawe anasema: Tena nitauazibu Yerusalema kwa mapigo yangu mane ya hukumu kali: vita, njaa, nyama wakali na ugonjwa mukali, nipate kuangamiza watu na nyama ndani yake!
Nami niliwatawanya kwa upepo mukali kati ya mataifa yote ambayo hawakuyajua. Hivyo inchi waliyoiacha ikabaki tupu; hapakuwa mutu yeyote aliyekaa mule; inchi hiyo ya kupendeza ikakuwa ukiwa.
Katika siku za Samugari mwana wa Anati, katika wakati wa Yaeli, makundi ya watu yalikoma kupita katika inchi, wasafiri walipitia njia za pembenipembeni.