Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Mutatumia nguvu zenu bure maana mashamba yenu hayatatoa mavuno na inchi yenu haitazaa matunda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:20
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Unapolima udongo, hautakupatia tena mazao yake. Utakuwa mukimbizi na mwenye kutangatanga katika dunia.”


Basi, Elia akaenda kujionyesha kwa Ahabu. Wakati huo, njaa ilikuwa kali sana kule Samaria.


basi miiba iote mule pahali pa ngano, na magugu pahali pa shayiri. Mwisho wa masemi ya Yobu.


Udongo wenye mboleo akaugeuza kuwa udongo usioweza kutoa, kwa sababu ya uovu wa wakaaji wake.


Wimbo wa safari za kidini: wa Solomono. Yawe asipoijenga nyumba, wanaoijenga wanajisumbua bure. Yawe asipoulinda muji, wanaoulinda wanakesha bure.


Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa, haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia. Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali, na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;


hata mukiifanya ikomae siku hiyohiyo muliyoipanda na kuifanya ichanue asubui hiyohiyo, mavuno yenu yatatoweka siku hiyo ya hasara na maumivu yasiyoweza kuponyeshwa.


Lakini mimi nikafikiri: Nimeshugulika bure, nimetumia nguvu zangu bure kabisa. Hata hivyo, Yawe atanipa haki yangu; mushahara wa kazi yangu uko kwa Mungu.


Walipanda ngano, lakini walivuna magugu; wamejichokesha kwa bure. Kwa sababu ya hasira kali ya Yawe, watasikia haya juu ya mavuno yao.


Kwa hiyo wakati wa mavuno nitaitwaa ngano yangu, nitaiondoa divai yangu kwa wakati wake. Nitamunyanganya nguo zangu za sufu na kitani, ambazo zilitumika kuufunika uchi wake.


nitawanyeshea mvua kwa wakati unaofaa, inchi ipate kuzaa mavuno kwa wingi, nayo miti ya mashamba matunda yake.


Yawe wa majeshi anasababisha juhudi za watu zipotelee katika moto, na mataifa yajishugulishe bure.


hali yenu ilikuwa namna gani? Mutu alifika kwenye fungu la ngano akingojea kupata vipimo makumi mbili, lakini kulikuwa vipimo kumi tu. Mutu alifika kwenye mutungi wa divai akingojea kujaza vyombo makumi tano, lakini kulikuwa makumi mbili tu.


Mimi nilipanda mbegu na Apolo alinyweshea maji, lakini Mungu ndiye aliyeiotesha.


Ninawaogopea, kwa maana inawezekana kwamba nimesumbuka bure kwa ajili yenu!


nayo hasira ya Yawe iwake juu yenu, naye afunge mbingu hata kusikuwe mvua, na inchi iache kutoa mazao yake, halafu muangamie upesi kutoka katika inchi nzuri ambayo Yawe anawapa.


Watoto wenu watalaaniwa na mazao yenu ya inchi; mifugo yenu italaaniwa isiongezeke.


Matunda yenu yote na mazao yenu katika mashamba vitashambuliwa na nzige.


Hasira yangu imewaka moto, inachoma mpaka chini kuzimu, itateketeza dunia na vinavyokuwa ndani yake, itaunguza misingi ya milima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ