Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”
“Mvua isiponyesha kwa sababu wametenda zambi mbele yako na unawaazibu, wakiomba wakielekea pahali hapa na kusifu jina lako, vilevile wakiziacha zambi zao na kukurudilia,
Ole wa Samaria, muji unaokuwa kama taji juu ya bonde kwenye udongo muzuri. Walevi wa ajabu wa Efuraimu wanajivuna kwa ajili yake, lakini utukufu wake utatoweka kama ua linalonyauka!
Uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.
Yawe anasema hivi: Wote wanaounga Misri mukono wataangamia, mashujaa wake wenye utukufu wataangamizwa, tangu Migidoli mpaka Sewene watu watauawa katika vita. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.
Ninawaambia ukweli: kulikuwa wajane wengi katika inchi ya Israeli katika siku za nabii Elia. Wakati ule, mvua ilifungwa isinyeshe kwa muda wa miaka mitatu na nusu na kukakuwa njaa kubwa katika inchi yote.
nayo hasira ya Yawe iwake juu yenu, naye afunge mbingu hata kusikuwe mvua, na inchi iache kutoa mazao yake, halafu muangamie upesi kutoka katika inchi nzuri ambayo Yawe anawapa.
Waaskari walioponyoka walipofika kwenye kambi, wazee wa Israeli walisema: “Kwa nini Yawe amewaacha Wafilistini watushinde leo? Tuende tulilete Sanduku la Agano la Yawe kutoka Shilo, kusudi aweze kwenda nasi katika vita na kutuokoa kutoka waadui zetu.”