Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Kiburi chenu nitakivunja kabisa kwa kufanya mbingu kule juu kuwa ngumu kama chuma na inchi yenu bila mvua ikuwe ngumu kama shaba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:19
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”


“Mvua isiponyesha kwa sababu wametenda zambi mbele yako na unawaazibu, wakiomba wakielekea pahali hapa na kusifu jina lako, vilevile wakiziacha zambi zao na kukurudilia,


Kweli, siku ya Yawe wa majeshi inakuja juu ya wote wenye kiburi na majivuno, juu ya wote wanaojitukuza,


Watainyoosha mikono yao kama mutu anayejaribu kuogelea, lakini pamoja na bidii yao, Yawe ataporomosha kiburi chao.


Amewaporomosha waliokaa pande za juu, muji wenye utukufu ameuangusha mpaka chini, ameutupa mpaka katika mavumbi.


Ole wa Samaria, muji unaokuwa kama taji juu ya bonde kwenye udongo muzuri. Walevi wa ajabu wa Efuraimu wanajivuna kwa ajili yake, lakini utukufu wake utatoweka kama ua linalonyauka!


Yawe anasema hivi: Hivi ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha watu Yuda na kiburi kikubwa cha watu wa Yerusalema.


Ndiyo maana manyunyu yamezuizwa kuanguka, wala mvua za mwisho hazijanyesha. Hata hivyo unakausha macho kama kahaba, wala hauna haya hata kidogo.


Uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.


Yawe anasema hivi: Wote wanaounga Misri mukono wataangamia, mashujaa wake wenye utukufu wataangamizwa, tangu Migidoli mpaka Sewene watu watauawa katika vita. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Nitaifanya inchi kuwa jangwa na tupu. Nitawaua mashujaa wake wenye kiburi. Milima ya inchi ya Israeli itakuwa jangwa na hakuna mutu atakayepita huko.


Nitaleta watu wa mataifa mabaya sana nao watarizi nyumba zao. Nitakikomesha kiburi chao, na pahali pao pa kutambikia patachafuliwa.


Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.


Ninawaambia ukweli: kulikuwa wajane wengi katika inchi ya Israeli katika siku za nabii Elia. Wakati ule, mvua ilifungwa isinyeshe kwa muda wa miaka mitatu na nusu na kukakuwa njaa kubwa katika inchi yote.


nayo hasira ya Yawe iwake juu yenu, naye afunge mbingu hata kusikuwe mvua, na inchi iache kutoa mazao yake, halafu muangamie upesi kutoka katika inchi nzuri ambayo Yawe anawapa.


Mbingu zitakauka kama shaba nyeusi bila mvua, na inchi itakuwa kama chuma.


Sanduku la Agano la Mungu lilitekwa, na wale wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi, wakauawa.


Waaskari walioponyoka walipofika kwenye kambi, wazee wa Israeli walisema: “Kwa nini Yawe amewaacha Wafilistini watushinde leo? Tuende tulilete Sanduku la Agano la Yawe kutoka Shilo, kusudi aweze kwenda nasi katika vita na kutuokoa kutoka waadui zetu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ