Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 basi, mimi nitafanya hivi: Nitawapiga kwa kuwaletea hofu kubwa ya rafla, kifua kikubwa na homa itakayowapofusha macho na kuwakondesha. Mutapanda mbegu zenu bila mafanikio maana waadui zenu ndio watakaozikula.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:16
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Ikiwa kuna njaa katika inchi, au ugonjwa mukali, ukosefu wa mvua, ugonjwa wa mimea, nzige au vidudu vingine, au ikiwa watu wako wameshambuliwa na waadui zao katika muji wao wowote, ikiwa kuna pigo lolote au ugonjwa wowote,


Hofu kubwa inamutisha kila upande, inamufuata katika kila hatua yake.


Mushale utachomolewa kutoka katika mwili wake; incha yake itatolewa katika mugongo wake ikingaa, vitisho vya kifo vitamupata.


basi nipande na mwingine akule, mazao yangu ya shamba yaongolewe.


Umuweke mwamuzi mubaya juu ya adui yangu; na anayemushitaki amupeleke mbele ya baraza.


Wanaangamizwa kwa rafla, wateketezwe kabisa kwa vitisho.


Basi, akatowesha siku zao kama pumzi, miaka yao kwa misiba ya rafla.


akawaambia: “Ikiwa mutaisikiliza kwa uaminifu sauti yangu mimi Yawe, Mungu wenu, kutenda yale yanayokuwa sawa mbele yangu, na kuheshimu amri na masharti yangu yote, basi, mimi sitawaletea yale magonjwa niliyowaletea Wamisri. Kwa sababu, mimi ni Yawe ninayewaponya ninyi.”


Yawe analaani nyumba za waovu, lakini anabariki makao ya wenye haki.


Hakuna! Mutajikunja tu kati ya wafungwa na kuangamia pamoja na wanaouawa katika vita. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Yawe ameapa kwa uwezo wake mukubwa, ameapa kwa nguvu yake akisema: Sitawapa tena waadui zako ngano yako; wala wageni hawatakunywa tena divai yako ambayo umeitoshea jasho.


Mufalme wa Yuda alipopata habari kwamba Waaramu wanashirikiana na Waisraeli, yeye pamoja na watu wote wa Yuda waliogopa na kutetemeka kama miti inayotikiswa na upepo.


Walipanda ngano, lakini walivuna magugu; wamejichokesha kwa bure. Kwa sababu ya hasira kali ya Yawe, watasikia haya juu ya mavuno yao.


Nimeamua kuleta aina ine za maangamizi juu yao: upanga kwa kuwaua, imbwa kwa kuwararua, ndege na nyama wa pori kwa kuwakula na kuwamaliza.


Wajane wao wamekuwa wengi kuliko muchanga wa bahari. Nao wamama wenye watoto vijana nimewaletea mwangamizaji muchana kati. Nimesababisha uchungu na vitisho viwapate kwa rafla.


Maana, Yawe anasema hivi: Nitakufanya ukuwe kitisho kwako wewe mwenyewe na kwa warafiki zako wote. Wao watauawa katika vita kwa upanga wa waadui zao, wewe ukiwa ukiangalia. Nitawatoa watu wote wa Yuda katika mikono ya mufalme wa Babeli, naye atawapeleka kuwa watumwa mpaka Babeli na kuwaua kwa upanga.


Watakula mazao yenu na chakula chenu; watawaua wana na wabinti zenu. Watachinja makundi yenu ya kondoo na ngombe; wataiharibu mizabibu yenu na miti yenu ya matunda ya tini. Miji yenu yenye kuzungukwa na kuta munayoitegemea, wataiharibu kwa silaha zao.


Mutavaa vitambaa kwa kichwa na viatu; hamutaomboleza, wala kulia. Kutokana na maovu yenu, mutaregea na kuugua, kila mutu na mwenzake.


Ewe mwanadamu! Uwaambie Waisraeli jambo hili: Ninyi munasema: Tumezidiwa na makosa na zambi zetu. Tunaregea kwa sababu yake! Tutaweza namna gani kuishi?


Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake.


Mutapanda mbegu, lakini hamutavuna. Mutakamua mafuta ya zeituni, lakini hamutatumia mafuta hayo. Mutakamua zabibu, lakini hamutakunywa divai hiyo.


Munapanda mbegu kwa wingi, lakini munavuna kidogo. Munakula, lakini hamushibi. Munakunywa divai, lakini hamutosheki. Munavaa nguo, lakini bado munasikia baridi. Mushahara wa mutumishi unakuwa kama umetumbukizwa katika mufuko uliotoboka.


Lakini juu ya wale watu ambao walikuja kupigana na Yerusalema, hizi ndizo hasara ambazo Yawe atawaletea: Miili yao itaoza wangali wazima; macho yao yataoza yakiwa kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza zikiwa katika vinywa vyao.


Nitawaazibu watoto wenu na ninyi wenyewe kutokana na uovu wenu, na kuzipakaa nyuso zenu mavi ya nyama wenu wa sadaka. Nitawafukuza mbali nami.


Watakula ngombe wenu na mazao yenu, mpaka muangamie. Hawatawaachia ngano, divai, mafuta, ngombe au kondoo mpaka wawaangamize.


Vita itasababisha vifo vingi inje, na ndani ya nyumba hofu itawatawala. Vijana wanaume na wanawake watauawa, hata wenye kunyonya na wazee wenye imvi.


Kuanguka katika mikono ya Mungu Mwenye Uzima ni jambo la kuogopa sana!


Malaika wa Yawe akaenda, akaikaa chini ya muti wa mwalo wa Yoasi Mwabiezeri, kule Ofura. Gideoni mwana wa Yoasi alikuwa anapepeta ngano ndani ya kikamulio cha kukamulia zabibu kusudi Wamidiani wasimwone.


Mutu wako ambaye sitamwangamiza kutoka mazabahu yangu atakuwa ameponyoka kusudi nipofushe macho yake, naye atakufa moyo na wazao wake watauawa kifo kibaya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ