Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Walawi 26:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 kama mukizarau masharti yangu na kuchukia kwa roho maagizo yangu mukiacha kutii amri zangu zote na kuvunja agano langu,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Walawi 26:15
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mwanaume yeyote asiyetahiriwa atatengwa na watu, maana atakuwa amevunja agano langu.”


Walikataa kutii masharti yake; hawakushika agano alilofanya na babu zao, walizarau maonyo yake, waliabudu sanamu zisizokuwa na maana hata wao wenyewe hawakukuwa na maana tena, walifuata desturi za mataifa yaliyowazunguka: walizarau amri za Yawe; wala hawakuzishika.


Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


Wewe unachukia maonyo, na maneno yangu haupendi kuyafuata.


Sasa basi, kama mukitii sauti yangu na kushika agano langu, mutakuwa watu wangu wachaguliwa kati ya mataifa yote, maana dunia yote ni yangu.


Kisha akatwaa kitabu cha agano la Yawe, akakisoma mbele ya watu, nao wakasema: Yale yote Yawe aliyoyasema tutayafanya, nasi tutakuwa watiifu.


mulikataa shauri langu, mukazarau maonyo yangu yote.


Kumwogopa Yawe ni musingi wa maarifa, lakini wapumbafu wanazarau hekima na mafundisho.


Kwa hiyo utasema: “Kwa nini nilichukia mafundisho? Kwa nini nilizarau ndani ya moyo wangu?


Watu wameichafua dunia maana wamezivunja sheria za Mungu, wamegeuka mbali na masharti yake, wamelivunja agano lake la milele.


Wameurudilia uovu wa babu zao ambao walikataa kusikiliza maneno yangu; wanaiabudu miungu mingine na kuitumikia. Watu wa Israeli na watu wa Yuda wamevunja agano nililofanya na babu zao.


Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na babu zao nilipowatoa kwa mukono wangu kutoka Misri; agano hilo walilivunja, ingawa mimi nilikuwa Bwana wao.


Sikiliza, ee dunia! Mimi nitawaletea watu hawa hasara kulingana na nia zao mbaya. Maana hawakuyajali maneno yangu, na mafundisho yangu nayo wameyakataa.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakutendea wewe Yerusalema kama unavyostahili. Wewe umekizarau kiapo, ukivunja agano.


Nitaweka makao yangu kati yenu, wala sitawaachilia.


Wakati watakapokuwa inje ya inchi yao, inchi hiyo itafurahia Sabato zake hapo itakapokuwa katika hali ya ukiwa. Wakati huo wao watatubu uovu wao wa kuzarau maagizo yangu na kuchukia masharti yangu.


Nitawarehemu na kuwajalia mupate watoto wengi na kuongezeka. Nami nitaliimarisha agano langu nanyi.


Ni lazima muniheshimu mimi kwa matendo yenu. Musiponisikiliza nitawaletea laana. Vitu vyote munavyopewa kwa mahitaji yenu nitavilaani. Na kweli nimekwisha kuvilaani, kwa sababu hamushuguliki hata kidogo na maagizo yangu.


Maana amekataa neno la Yawe na kuvunja moja kati ya amri zake. Mutu huyo atatengwa mbali kabisa; na lazima ya kifo chake itakuwa juu yake mwenyewe.


‘Muangalie, ninyi wenye kuzarau, mupigwe na mushangao na mutoweke! Maana katika siku hizi nitafanya jambo ambalo ninyi musingeweza kusadikia hata wangewaelezea.’ ”


Kwa maana wale wanaoshugulika na hali ya kimwili ni waadui za Mungu; hawatii sheria ya Mungu wala hawawezi kuitii.


Yawe akamwambia Musa: “Umekaribia sasa kuaga dunia, na kisha kufa kwako, watu wataanza kuniacha na kuendea miungu mingine ya inchi hiyo ambamo watakwenda kuishi. Wataniacha na kuvunja agano nililoagana nao.


Basi kwa hiyo, yeye anayekataa mafundisho haya hamukatai mutu, lakini anamukataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mutakatifu.


Agano lile halitakuwa sawa na lile nililofanya na babu zao siku nilipowakamatia kwenye mukono na kuwaondoa toka inchi ya Misri. Kwa sababu hawakushika lile agano, kwa hiyo vilevile sikuwashugulikia. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo.


Lakini kama hamutasikiliza sauti ya Yawe, mukiasi amri yake, basi yeye atapambana nanyi pamoja na mufalme wenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ